Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 4:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Lakini sisi ni watu wa Mungu. Mutu anayemujua Mungu anatusikiliza; yule asiyemujua Mungu hatusikilizi. Basi ni kwa njia hii tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho ya udanganyifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 4:6
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye akajibu: ‘Nitakwenda na kuwasukuma manabii wake wote waseme uongo.’ Yawe akamwambia: ‘Wewe utamushawishi na utashinda; kwenda kufanya hivyo.’


Yawe amewamwangia roho ya usingizi; macho yenu yasipate kuona enyi manabii, amefunika vichwa vyenu enyi wenye kupata maono.


Hakika anayesema hivyo hajapata kuona mwangaza. Lakini ninyi mushike lile agizo na mafundisho ya Mungu.


Watu wangu wanaomba shauri kutoka kwa muti; kijiti chao cha kuaguza ndicho kinachowapa shauri. Nia ya kufanya uzinzi imewapotosha; wamefanya uzinzi kwa kufuata miungu mingine, wakaniacha mimi Mungu wao.


Kama mutu angetokea akitangaza maneno matupu ya uongo na kusema “Ninawatabiria divai na pombe kwa wingi”, muhubiri wa namna hiyo angependwa na watu hawa!


Lakini kwa upande wangu, nimejazwa nguvu na roho ya Yawe; nimejaliwa kufuata sheria ya Mungu na kuwa na uwezo niwatangazie wazao wa Yakobo kosa lao, niwaambie Waisraeli zambi yao.


“Baba yangu, umeweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana na yeyote ambaye Mwana anataka kumujulisha kwake.”


Niko na kondoo wengine wasiokuwa wa kundi hili. Ninapaswa vilevile kuwaleta, nao watasikia sauti yangu, na kutakuwa kundi moja na muchungaji mumoja.


Kondoo wangu wanasikia sauti yangu, ninawajua, nao wananifuata.


Zamu anamufungulia mulango na kondoo wanasikia sauti yake. Naye anawaita kondoo wake kila mumoja kwa jina lake na kuwapeleka inje.


Kweli, kweli ninawaambia: mutu anayemupokea yule ninayemutuma, ananipokea mimi vilevile; na mutu anayenipokea, anamupokea yule aliyenituma.”


naye ndiye Roho wa ukweli. Dunia haiwezi kumupokea, kwa sababu haimwoni wala haimujui. Lakini munamujua, kwa maana anaishi pamoja nanyi naye anakuwa ndani yenu.


“Wakati Musaidizi nitakayewatumia toka kwa Baba atakapokuja, atanishuhudia mimi. Yeye ni Roho wa ukweli, naye anakuja toka kwa Baba.


Lakini wakati yule Roho wa ukweli atakapokuja, atawaongoza ninyi kufuata ukweli wote kabisa. Yeye hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, lakini atasema tu yale atakayosikia, naye atawatangazia ninyi habari za mambo yatakayokuja.


Halafu Pilato akamwuliza: “Ni kusema wewe ni mufalme?” Yesu akamujibu: “Wewe umesema kwamba mimi ni mufalme. Mimi nimezaliwa na kuja katika dunia kusudi nishuhudie ukweli. Wote wanaokuwa upande wa ukweli, wananisikiliza mimi.”


Yesu akawaambia tena: “Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma, mimi ninawatuma ninyi vilevile.”


Basi wakamwuliza: “Baba yako yuko wapi?” Yesu akajibu: “Hamunijui mimi wala hamumujui Baba yangu. Kama mungenijua mimi, mungemujua Baba yangu vilevile.”


Yesu akawajibu: “Ninyi munatoka hapa chini, lakini mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa dunia hii, lakini mimi si wa dunia hii.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Kristo Yesu, niliyeitwa na Mungu kuwa mutume na niliyewekwa kwa kazi ya kutangaza Habari Njema yake.


kama vile ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Mungu ameifanya mioyo yao kuwa migumu, macho yao yasipate kuona na masikio yao yasipate kusikia, na ni hivi wanavyokuwa hata leo.”


Kama mutu akizani kwamba yuko na zawadi ya unabii au zawadi ingine ya Roho, anapaswa kujua kwamba maneno haya ninayowaandikia ninyi ni amri ya Bwana.


Ninyi munaangalia tu namna vitu vinavyoonekana kwa inje. Mutu yeyote anayejiaminia kwamba yeye ni wa Kristo, inafaa afikiri tena yeye mwenyewe mambo haya: ikiwa yeye ni wa Kristo sisi vilevile ni wa Kristo.


katikati ya ndimi za moto kwa kuazibu wale wanaokataa kumujua Mungu na wale wasiokubali Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.


Roho Mutakatifu anasema wazi kwamba katika nyakati za mwisho, watu wengine watapotoka katika imani yao na kufuata roho za udanganyifu na mafundisho ya pepo.


Ninataka mukumbuke maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu na ile amri ya Bwana na Mwokozi muliyotolewa na mitume wenu.


Wapendwa wangu, musimwaminie kila mutu anayesema kwamba yuko na Roho wa Mungu, lakini mumupime kwa kuhakikisha kama roho yule anatoka kwa Mungu. Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea katika dunia.


Lakini ninyi, watoto wangu, muko watoto wa Mungu, nanyi mumewashinda manabii wa uongo; maana roho anayekaa ndani yenu ni mwenye uwezo kuliko yule anayekaa ndani ya watu wa dunia.


Mutu asiyekuwa na upendo hamujui Mungu kwa maana Mungu ni upendo.


Tunajua kwamba sisi ni watoto wa Mungu ingawa dunia yote inatawaliwa na yule Mwovu.


Lakini ninyi wapendwa wangu, mukumbuke maneno yaliyosemwa zamani na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ