21 Basi hii ndiyo amri tuliyopewa na Kristo: yule anayemupenda Mungu anapaswa kumupenda ndugu yake vilevile.
Usijilipize kisasi au kuwa na kinyongo juu ya wazao wa watu wako lakini umupende mwenzako kama vile unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ni Yawe.
“Mumesikia kwamba imesemwa hivi: ‘Umupende mwenzako, lakini umuchukie adui yako.’
Naye akajibu: “Ni yule aliyemusikilia huruma.” Halafu Yesu akamwambia: “Kwenda, nawe ufanye sawa sawa.”
Hii ndiyo amri ninayowapa: mupendane ninyi kwa ninyi kama ninavyowapenda.
Kwa maana Sheria yote inafungwa katika amri hii moja: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda mwenyewe.”
Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.
Na kuelekea upendo wa wandugu waamini, si lazima kwenu kuwaandikia neno lolote, kwa maana Mungu yeye mwenyewe amewafundisha ninyi kupendana.
Kwa kumaliza, ninyi wote mukuwe na mawazo na nia moja, mupendane kama wandugu waamini, mukuwe wema na wanyenyekevu.
Na zaidi ya yote mudumu katika upendo ninyi kwa ninyi, maana upendo unafunika zambi nyingi.
Wapenzi, siwaandikii amri mupya, lakini ile ya zamani muliyoijua tangia mbele. Na amri hiyo ya zamani ni lile neno mulilosikia.
Kwa maana huu ndio ujumbe muliosikia tangia mbele: tupendane sisi kwa sisi.
Sisi tunajua kwamba tumeponyoka lufu na kupata uzima kwa sababu tunawapenda wandugu zetu. Mutu asiyekuwa na upendo ni kama mufu.
Watoto wangu, upendo wetu usikuwe wa masemi tu; lakini unapaswa kuwa upendo wa kweli na unaoonekana kwa matendo.
Amri yake ndiyo hii tuamini jina la Mwana wake Yesu Kristo na tupendane sisi kwa sisi kama vile Kristo alivyotuamuru.
Wapendwa wangu, ikiwa Mungu alitupenda sisi namna ile, sisi vilevile tunapaswa kupendana.