Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 4:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Hivi upendo umekamilishwa ndani yetu, kusudi tupate kuwa na tumaini kwa Siku ile ya hukumu. Kwa sababu maisha yetu katika dunia hii yanafanana na maisha ya Yesu Kristo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 4:17
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kweli ninawaambia: kwa Siku ya hukumu, watu wa muji ule wataazibiwa vikali zaidi kuliko watu wa muji wa Sodoma na wa Gomora.


Lakini inatosha kwa mwanafunzi kufanana na mwalimu wake na mutumishi kufanana na bwana wake. Ikiwa wanamwita mukubwa wa jamaa Belzebuli, hawatakosa kuwaita watu wa jamaa yake kwa majina mabaya zaidi.


Kwa hiyo ninawaambia kwamba kwa Siku ya hukumu, ninyi mutaazibiwa zaidi kuliko muji wa Tiro na wa Sidona.


Kwa hiyo ninawaambia kwamba kwa Siku ya hukumu, wewe utaazibiwa zaidi kuliko watu wa Sodoma!”


“Ninawaambia wazi kwamba kwa Siku ya hukumu, watu watasamba kila neno lisilokuwa na maana walilosema.


Mukumbuke maneno niliyowaambia kwamba mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake. Kama walinitesa mimi, watawatesa ninyi vilevile. Na kama walishika maneno yangu, watashika maneno yenu vilevile.


Nami nimewapa utukufu ulionipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja.


Kwa maana wale Mungu aliowachagua tangu zamani, ndio aliofanya mupango juu yao tangu zamani, apate kuwafananisha na Mwana wake, kusudi Mwana wake akuwe muzaliwa wa kwanza wa wandugu wengi.


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Basi unaona kwamba imani yake ilionekana kwa njia ya matendo yake na kwa njia hiyo ikapata kukamilishwa.


Basi, ni kusema kwamba Bwana anajua namna ya kuwaokoa wenye kumwogopa katika majaribu. Lakini anangojea kuwaazibu watu wabaya kwa Siku ile ya hukumu.


Lakini kwa nguvu ya neno lile lile, mbingu na dunia za sasa zimewekwa akiba kwa kuteketezwa kwa moto. Zinalindwa kwa ajili ya Siku ile ambayo watu wabaya watahukumiwa na kuangamizwa.


Na sasa watoto wangu, mukae ndani yake kusudi tukuwe na tumaini hakika wakati atakapotokea, na kutosikia haya mbele yake siku atakaporudi.


Lakini yule anayetii neno la Mungu yuko na upendo kamili wa Mungu ndani yake. Hili ndilo jambo linalotuonyesha kwamba sisi tunaungana na Mungu:


mutu yeyote anayesema kwamba anaungana na Mungu anapaswa kuishi sawa vile Yesu alivyoishi.


Muangalie namna Baba alivyoonyesha upendo wake kwetu hata tupate kuitwa watoto wa Mungu! Na kwa hakika sisi ndio wao! Ndiyo maana watu wa dunia hawatutambui, kwa sababu hawakumujua Mungu.


Basi, kila mutu anayekuwa na tumaini hili katika Kristo anajisafisha mwenyewe kama vile Kristo anavyokuwa safi.


Watoto wangu, mutu asiwadanganye! Mutu anayetenda mambo ya haki ni mwenye haki kama vile Kristo ni mwenye haki.


Hakuna hata mutu aliyekwisha kumwona Mungu wakati wowote. Tukipendana sisi kwa sisi, Mungu anaungana nasi na upendo wake unakamilika ndani yetu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ