Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?
nao wakamwambia yule mwanamuke: “Sasa tunaamini, si kwa sababu ya maneno uliyotuambia tu, lakini kwa sababu tumesikia sisi wenyewe na tunajua hakika kwamba huyu ni Mwokozi wa dunia.”
Nimewaandikia barua hii fupi nikisaidiwa na Sila, ninayemujua kuwa ndugu mwaminifu. Ninataka kuwatia moyo na kushuhudia kwenu kwamba mambo hayo yanayoelekea neema ya Mungu ni ya kweli; nanyi musikose kushikamana nayo.
Na huu ndio upendo: si kwamba sisi tulimupenda Mungu, lakini kwamba ni yeye ndiye aliyetupenda hata akatuma Mwana wake kama vile sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu.