11 Wapendwa wangu, ikiwa Mungu alitupenda sisi namna ile, sisi vilevile tunapaswa kupendana.
Naye akajibu: “Ni yule aliyemusikilia huruma.” Halafu Yesu akamwambia: “Kwenda, nawe ufanye sawa sawa.”
Ninawapa amri mupya: mupendane ninyi kwa ninyi. Kama mimi nilivyowapenda, nanyi mupendane vilevile.
Mutupilie mbali nanyi nia zote za uadui, chuki, kasirani, fujo na masingizio. Mutupilie mbali ubaya wa kila namna!
Muvumiliane na kusameheana ninyi kwa ninyi wakati wowote mutu anapokuwa na neno la kumushitaki mwingine. Munapaswa kusameheana kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.
Wapenzi, siwaandikii amri mupya, lakini ile ya zamani muliyoijua tangia mbele. Na amri hiyo ya zamani ni lile neno mulilosikia.
Kwa maana huu ndio ujumbe muliosikia tangia mbele: tupendane sisi kwa sisi.
Amri yake ndiyo hii tuamini jina la Mwana wake Yesu Kristo na tupendane sisi kwa sisi kama vile Kristo alivyotuamuru.
Wapendwa wangu, tupendane, kwa maana upendo unatoka kwa Mungu. Kila mutu anayekuwa na upendo ni mutoto wa Mungu naye anamujua Mungu.
Na sasa Mama, ninakusihi: tupendane. Basi hii si amri mupya ninayokuandikia, lakini ni amri ile tuliyopokea tangu mwanzo.