Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Wapendwa wangu, musimwaminie kila mutu anayesema kwamba yuko na Roho wa Mungu, lakini mumupime kwa kuhakikisha kama roho yule anatoka kwa Mungu. Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea katika dunia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 4:1
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yule muzee wa Beteli akamwambia: “Mimi vilevile ni nabii kama wewe, na Yawe amesema nami kwa njia ya malaika akisema: ‘Umurudishe kwako, akule chakula na kunywa maji.’ ” Lakini yule nabii muzee alikuwa anamudanganya tu.


Mujinga anaamini kila kitu anachoambiwa, lakini mwenye akili anachunguza hatua zake zote.


Naye Yawe akaniambia: Hao manabii wanatoa unabii wa uongo kwa jina langu. Mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi yao hayana maana yoyote, wao wanajitungia uongo wenyewe.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Musisikilize maneno manabii wanaowatabiria; wanawapa matumaini ya uongo. Yale wanayowaambia ni maono ya mioyo yao wenyewe. Hayakutoka katika kinywa cha Yawe.


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


“Kwa hiyo mutu akiwaambia: ‘Kristo yuko hapa!’ au ‘Yuko kule!’ musimusadiki.


“Sababu gani ninyi wenyewe hamuwezi kujiamulia jambo la haki?


Yesu akawajibu: “Muangalie vizuri, musidanganywe. Watu wengi watakuja wakijiita kwa jina langu, wakisema kwamba wao ndio Kristo, nao wakati umetimia. Ingawa vile, musiwafuate.


Watu hao walikuwa wenye nia nzuri zaidi kuliko watu wa Tesalonika; nao walipokea Neno la Mungu kwa hamu kubwa. Kila siku walichunguza Maandiko Matakatifu wapate kujua kwamba maneno Paulo aliyosema yalikuwa ya haki.


Ninajua kwamba nyuma ya kuondoka kwangu, imbwa wakali wa pori wataingia katikati yenu, nao hawatahurumia kundi lile.


Mwingine anapewa uwezo wa kufanya miujiza, mwingine zawadi ya kutabiri, na mwingine uwezo wa kutambua roho ya uongo na Roho wa ukweli. Mwingine alipewa uwezo wa kusema luga za ajabu na mwingine uwezo wa kutafsiri luga zile.


Na kwa upande wa wale wanaotabiri, wanaweza kusema wawili au watatu na watu wengine wapime yale wanayosema.


Lakini muchunguze kila jambo na kushika lile linalokuwa jema.


musifazaike upesi wala kuogopa kwamba Siku ya kurudi kwa Bwana imekwisha kutimia. Inawezekana munafahamu mambo yale kwa njia ya unabii, mahubiri na barua inayosemeka kwamba imetoka kwetu.


Roho Mutakatifu anasema wazi kwamba katika nyakati za mwisho, watu wengine watapotoka katika imani yao na kufuata roho za udanganyifu na mafundisho ya pepo.


Lakini watu waovu na wadanganyifu wataendelea katika maovu, wakipotosha watu wengine na kujipotosha wenyewe.


Zamani manabii wa uongo walitokea kati ya watu, na ndivyo hivyo walimu wa uongo watakavyotokea kati yenu. Watu hawa wataingiza mafundisho mabaya sana ya uongo kwa siri, wakimukataa hata Bwana aliyewakomboa na kujiletea maangamizi upesi.


Watoto wangu, huu ni wakati wa mwisho. Mulisikia habari kwamba mupinga Kristo atakuja, lakini hata sasa wapinga Kristo wengi wametokea. Na kwa hiyo tunajua kwamba ni wakati wa mwisho.


Wapenzi, siwaandikii amri mupya, lakini ile ya zamani muliyoijua tangia mbele. Na amri hiyo ya zamani ni lile neno mulilosikia.


Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea katika dunia. Watu hawa hawakubali kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili wa kimutu. Yule asiyekubali vile ni mudanganyifu na mupinga Kristo.


Mupendwa wangu, usifuate mufano mubaya, lakini ufuate mufano muzuri. Mutu anayetenda mema ni mutoto wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hashirikiani na Mungu.


Ninajua matendo yako na taabu yako na uvumilivu wako. Ninajua kwamba hauwezi kuwakubali watu waovu. Umewapima wale wanaojiita mitume, kumbe si mitume, nawe ukatambua kwamba ni wasema uongo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ