Kwa maana tamaa za kimwili zinapingana na tamaa za Roho Mutakatifu. Na tamaa za Roho zinapingana na tamaa za kimwili. Hao wawili wanapingana hata munashindwa kufanya sawa vile munavyotaka.
Kwa maana mumezaliwa upya, kwa nguvu za neno la Mungu lenye uzima na linalodumu hata milele. Nanyi si kama watoto waliozaliwa na wazazi wenye mwili huu unaokuwa wa kufa, lakini watoto waliozaliwa kwa nguvu ya uzazi usioweza kufa.
Mupendwa wangu, usifuate mufano mubaya, lakini ufuate mufano muzuri. Mutu anayetenda mema ni mutoto wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hashirikiani na Mungu.