Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 3:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Kila mutu anayefanya zambi anavunja sheria ya Mungu, kwa sababu kufanya zambi ni kuvunja sheria.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 3:4
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

kama watakapokuwa kule katika uhamisho wakijifikiri ndani yao wenyewe na kukugeukia, kama katika ile inchi ya uhamisho wakikusihi na kusema ‘Tumetenda zambi; tumepotoka na kufanya maovu’,


Saulo alikufa kwa sababu ya kutokuwa mwaminifu; hakukuwa mwaminifu maana hakutii neno la Yawe na alikwenda kwa mwaguzi kumwomba shauri,


Halafu Roho wa Mungu akamujaza Zakaria mwana wa kuhani Yoyada, naye akasimama mbele ya watu kwa pahali palipokuwa juu kidogo, akawaambia: “Yawe anauliza: Kwa nini mumevunja sheria zake? Sasa hamuwezi kufanikiwa! Kwa vile mumemwacha, naye vilevile amewaacha!”


Alikamatwa kwa kinguvu, akahukumiwa na kupelekwa kuuawa; na hakuna mutu aliyejali mambo yanayomupata. Alifukuzwa kutoka inchi ya wanaokuwa wazima, kwa sababu ya makosa ya watu wangu.


Waisraeli wote wameiasi sheria yako, wamekuacha wakakataa kukutii. Kwa sababu tumekukosea, tumemwangiwa laana na viapo vilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, mutumishi wako.


Maana amekataa neno la Yawe na kuvunja moja kati ya amri zake. Mutu huyo atatengwa mbali kabisa; na lazima ya kifo chake itakuwa juu yake mwenyewe.


Ni kwa hiyo mutu yeyote atakayevunja hata amri moja inayokuwa ndogo kuliko zingine zote, na kuwafundisha watu wengine kufanya kama yeye, huyu atahesabiwa kuwa mudogo katika Ufalme wa mbinguni. Lakini yule atakayezishika na kuzifundisha wengine, huyu atahesabiwa kuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni.


Halafu Paulo akamwambia: “Mungu yeye mwenyewe atakupiga kofi, wewe unayeonekana kwa inje kama ukuta uliopakaliwa chokaa! Wewe unaikaa pale kwa kunihukumu kufuatana na Sheria. Lakini wewe mwenyewe unaivunja kwa kuamuru wanipige!”


Kwa sababu hakuna mutu atakayehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa kuwa anatii Sheria, maana Sheria inamusaidia mutu tu kwa kutambua kwamba amefanya zambi.


Kwa sababu Sheria inaamusha kasirani ya Mungu. Lakini Sheria haingekuwa, kuvunja Sheria hakungekuwa vilevile.


Ninaogopa kwamba kwa safari yangu ingine, Mungu wangu atanifanya tena kuwa mwenye haya mbele yenu. Nami nitalia kwa ajili ya watu wengi waliofanya zambi zamani nao hawakugeuka toka katika uasherati, uzinzi na tamaa mbaya walizofanya.


Nao wakiomba kwa imani, mugonjwa yule atapona, kwa kuwa Bwana atamurudishia afya yake. Na ikiwa amefanya zambi, atasamehewa.


Kila tendo lisilokuwa la haki ni zambi, lakini kuna zambi isiyoleta kifo.


Saulo akamwambia Samweli: “Nimetenda zambi. Nimeasi amri ya Yawe na amri yako, kwa sababu niliwaogopa watu, nikawatii wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ