Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 3:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Amri yake ndiyo hii tuamini jina la Mwana wake Yesu Kristo na tupendane sisi kwa sisi kama vile Kristo alivyotuamuru.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 3:23
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na ya pili inayofanana nayo ni hii: ‘Umupende mwenzako kama vile unavyojipenda mwenyewe.’


Halafu wingu likatokea na kuwafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa. Mumusikilize!”


Lakini wamoja waliomupokea, ndio wale waliomwamini, aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu.


Ninawapa amri mupya: mupendane ninyi kwa ninyi. Kama mimi nilivyowapenda, nanyi mupendane vilevile.


Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Musifazaike; mumwamini Mungu, na muniamini mimi vilevile.


Hii ndiyo amri ninayowapa: mupendane ninyi kwa ninyi kama ninavyowapenda.


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


Wakati ule Yesu alipokuwa Yerusalema kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini kwa sababu waliona vitambulisho alivyofanya.


Anayemwamini Mwana hahukumiwi, lakini asiyemwamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.


Yesu akawajibu: “Hii ndiyo kazi ya Mungu: mumwamini yule aliyemutuma.”


Nao wakajibu: “Umwamini Bwana Yesu, nawe utaokolewa pamoja na watu wote wa nyumba yako.”


Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.


Na kuelekea upendo wa wandugu waamini, si lazima kwenu kuwaandikia neno lolote, kwa maana Mungu yeye mwenyewe amewafundisha ninyi kupendana.


Neno hili ni la kuaminiwa nalo linastahili kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja katika dunia kwa kuokoa wenye zambi. Na mimi ni wa kwanza mwenye zambi kati yao,


Ninyi mumekwisha kutakaswa kwa njia ya kutii neno la kweli kwa kuwapenda wandugu zenu pasipo unafiki. Basi mupendane kabisa, kwa moyo wenu wote.


Na zaidi ya yote mudumu katika upendo ninyi kwa ninyi, maana upendo unafunika zambi nyingi.


Wapenzi, siwaandikii amri mupya, lakini ile ya zamani muliyoijua tangia mbele. Na amri hiyo ya zamani ni lile neno mulilosikia.


Kwa maana huu ndio ujumbe muliosikia tangia mbele: tupendane sisi kwa sisi.


Kila mutu anayesema kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaungana naye, na mutu yule anaungana na Mungu.


Basi hii ndiyo amri tuliyopewa na Kristo: yule anayemupenda Mungu anapaswa kumupenda ndugu yake vilevile.


Ninawaandikia maneno yale, ninyi wenye kuamini kwa jina la Mwana wa Mungu, mupate kujua kwamba muko na uzima wa milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ