Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 3:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Mutu akiwa na mali ya dunia hii naye akimwona ndugu yake katika hitaji, lakini hataki kumusikilia huruma, mutu yule anaweza kusema kwamba anamupenda Mungu?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 3:17
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutu mwenye haki anajali nyama wake, lakini huruma za waovu ni kutesa tu.


Anayemutesa muzaifu anamutukana Muumba wake, lakini anayemwonea huruma mukosefu anamutukuza Mungu.


Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.


Anayekataa kusikia kilio cha masikini hatasikilizwa atakapolilia musaada.


Anayekataa kuisikia sheria, yule, hata maombi yake, ni chukizo kwa Mungu.


Naye akawajibu: “Mwenye kuwa na kanzu mbili atoe moja kwa yule asiyekuwa na kitu, na anayekuwa na vyakula afanye hivi vilevile.”


Kwa maana munajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ingawa alikuwa tajiri, yeye mwenyewe alijifanya masikini kwa ajili yenu, kusudi mupate kuwa watajiri kwa njia ya umasikini wake.


Tena, musisahau kutenda mema na kusaidiana, maana sadaka za namna hii zinamupendeza Mungu.


Kwa mufano: kaka au dada fulani akikosewa nguo au chakula,


itakuwa na faida gani, kama mumoja wenu anamwambia: “Mwende vizuri, mukaote moto na kushiba,” lakini hamusaidii na kitu chochote?


Kama mutu akisema “Ninamupenda Mungu,” naye anamuchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana yule asiyemupenda ndugu yake anayemwona, hawezi kumupenda Mungu asiyemwona.


Mutu yeyote anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, yeye ni mutoto wa Mungu; na kila mutu anayemupenda baba anamupenda mwana wake vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ