1 Yoane 3:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
16 Sisi tumetambua upendo kwa njia hii: Yesu Kristo alitoa uzima wake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kutoa uzima wetu kwa ajili ya wandugu zetu.
Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.
Wao walijitolea kufa kwa kuokoa maisha yangu. Ninawashukuru, wala si mimi peke yangu tu, nayo makanisa yote ya inchi za watu wa mataifa wanawashukuru vilevile.
Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.
kwa sababu yeye alikuwa karibu kufa kwa ajili ya kazi ya Kristo. Alihatarisha maisha yake kwa kuja kuniletea musaada ule ambao ninyi wenyewe musingeweza kunipatia.
Sisi tunawapenda sana hata tumekuwa tayari, si kuwatolea Habari Njema ya Mungu tu, lakini kutoa maisha yetu kwa ajili yenu vilevile. Ni vile kwa sababu ninyi mumekuwa kweli wapendwa wetu.
Kwa maana munajua namna gani mulivyokombolewa toka katika tabia za ovyo ovyo mulizoambukizwa na babu zenu. Hamukukombolewa kwa njia ya vitu vinavyoharibika kama vile feza au zahabu.
Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.
Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.
na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.
Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.