Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mutu akijidai kwamba anamujua Mungu, lakini hashiki amri zake, yeye ni mwongo, nao ukweli hauko ndani yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 2:4
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Kufuatana na hiyo, kuna watu wengi hasa kati ya Wayuda walioamini, wanaokuwa waasi, wakatetea na wadanganyifu.


Wanajidai kwamba wanamujua Mungu, lakini wanamukana kwa matendo yao. Wao ni wenye machukizo, waasi hata hawafai kwa kufanya kazi yo yote nzuri.


Tukisema kwamba hatukutenda zambi, tunamugeuza Mungu kuwa mwongo, na ukweli wa neno lake si ndani yetu.


Tukisema kwamba tunashirikiana naye, lakini tunaishi katika giza, tunasema uongo, nayo matendo yetu si ya kweli.


Tukisema kwamba hatuna zambi, tunajidanganya sisi wenyewe, wala ukweli hauko ndani yetu.


Sisi tunatambua kwamba tunamujua Mungu ikiwa tunashika amri zake.


Mutu anayesema kwamba anaishi katika mwangaza, lakini anamuchukia ndugu yake, yeye angali anaishi katika giza.


Basi kila mutu anayeungana naye hafanyi tena zambi; lakini kila mutu anayefanya zambi hakumwona wala kumujua.


Kama mutu akisema “Ninamupenda Mungu,” naye anamuchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana yule asiyemupenda ndugu yake anayemwona, hawezi kumupenda Mungu asiyemwona.


Wapendwa wangu, tupendane, kwa maana upendo unatoka kwa Mungu. Kila mutu anayekuwa na upendo ni mutoto wa Mungu naye anamujua Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ