Musitumikie chakula kinachoharibika, lakini mutumikie chakula kinachodumu na kuleta uzima wa milele. Mwana wa Mutu atawapa ninyi chakula hiki, kwa sababu Mungu Baba ametoa uhakikisho juu yake.”
Hivi kama vile zambi ilivyotawala na kuleta kifo, hivi vilevile neema ya Mungu itawale kwa njia ya haki na kuleta uzima wa milele, kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu.
Anayepanda kwa kupendeza hali yake ya kimwili, atavuna matunda yanayotokana na hali ile, nayo ni lufu. Lakini anayepanda kwa kupendeza Roho Mutakatifu, atavuna matunda yanayotokana na Roho yule, nayo ni uzima wa milele.
lakini kwa sababu hiyo Mungu amenihurumia. Alifanya vile kusudi kwa njia yangu mimi ninayekuwa mutenda zambi wa kwanza, Yesu Kristo apate kuonyesha uvumilivu wake. Na hivi mimi nipate kuwa mufano kwa wote watakaoamini nyuma na kupata uzima wa milele.
Uzima huu ulipotokea, sisi tuliuona. Kwa sababu hii tunaushuhudia na kuwatangazia habari za huo uzima wa milele, uliokuwa pamoja na Baba na ulioonyeshwa kwetu.
Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.