Halafu Pilato akamwuliza: “Ni kusema wewe ni mufalme?” Yesu akamujibu: “Wewe umesema kwamba mimi ni mufalme. Mimi nimezaliwa na kuja katika dunia kusudi nishuhudie ukweli. Wote wanaokuwa upande wa ukweli, wananisikiliza mimi.”
Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.
Ijapokuwa mumekwisha kujua kabisa mambo haya yote, ninataka kuwakumbusha namna Bwana alivyowaokoa Waisraeli kutoka katika inchi ya Misri, lakini kisha, akawaangamiza wale waliokataa kuamini.