Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 2:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Dunia inapita pamoja na tamaa zake, lakini mutu yule anayefanya mapenzi ya Mungu anaishi milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 2:17
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe uliumba dunia tokea zamani, mbingu ni kazi ya mikono yako.


Unifundishe kutimiza mapenzi yako, maana wewe ni Mungu wangu! Roho wako muzuri aniongoze katika njia sawa.


Kumbe umenipimia maisha mafupi sana! Maisha yangu si kitu mbele yako. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Kwa hasira yako maisha yetu yanatoweka, yanaisha kama pumzi.


Upepo mukali unapopita na mwovu anatoweka, lakini mwenye haki anaimarishwa milele.


Kati ya hawa wawili ni nani aliyefanya sawa na mapenzi ya baba yake?” Wale wakubwa wakajibu: “Ni yule wa kwanza.” Na Yesu akawaambia: “Kweli ninawaambia: Walipishaji wa kodi pamoja na makahaba wataingia mbele yenu katika Ufalme wa Mungu.


Mbingu na dunia vitatoweka, lakini maneno yangu hayatabadilika hata kidogo.


“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Kwa sababu mutu yeyote anayefanya mapenzi ya Mungu, huyu ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”


lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”


Huu ndio mukate ulioshuka toka mbinguni, nao si kama mukate ule babu zenu waliokula katika jangwa na kufa. Anayekula mukate huu ataishi milele.”


Kama mutu akitaka kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu, au kama ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe.


Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.


Wale wanaotumia mali ya dunia hii wakuwe kama vile wasioitumia. Kwa maana dunia hii inakaribia kupita.


Kwa sababu hii hatuchoki kuwaombea ninyi, tangu siku tuliposikia habari zenu. Tunamwomba Mungu awawezeshe kujua kabisa mapenzi yake na kuwajaza hekima na akili inayotoka kwa Roho wake.


Mwanainchi mwenzenu Epafra anawasalimia vilevile. Yeye ni mutumishi wa Yesu Kristo, hachoki kwa kuwaombea ninyi, kusudi musimame imara mukikomaa kiroho na kuwa tayari kwa kutimiza kabisa mapenzi ya Mungu.


Kitu Mungu anachotaka ni kwamba mukuwe watakatifu na muepuke mambo ya uasherati.


Mumushukuru Mungu katika mambo yote. Kwa maana hayo ndiyo mambo Mungu anayotaka mufanye katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.


Ninyi hamujui namna gani maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Kwa maana ninyi ni kama muvuke unaoonekana kwa wakati kidogo, kisha unatoweka.


Ninyi ambao kwa imani munalindwa salama kwa nguvu za Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa kwa mwisho wa nyakati.


Sasa, musiishi tena kufuatana na tamaa za kimutu, lakini muishi kufuatana na mapenzi ya Mungu kwa muda unaowabakilia kwa kukaa katika dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ