Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 2:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Kwa maana kila kitu kinachokuwa katika dunia, kama vile tamaa ya kimwili, tamaa ya macho, na majivuno ya maisha, hivi vyote havitoki kwa Baba, lakini vinatoka katika dunia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 2:16
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, mwanamuke alipoona kwamba muti ule ni muzuri kwa chakula, unavutia macho, na kwamba unafaa kwa kupata hekima, akachuma tunda lake, akakula, akamupa mume wake aliyekuwa pamoja naye, naye vilevile akakula.


wana wa Mungu wakaona kwamba wale wabinti za watu ni wazuri, wakawatwaa wale waliowapendeza kuwa wake zao.


Nimejizuiza kabisa mimi mwenyewe, macho yangu yasimwangalie binti kwa tamaa.


Kiburi kimekuwa kama mukufu katika shingo, mateso makali ni kama nguo yao.


Walimujaribu Mungu kwa makusudi; wakidai wapewe chakula walichotaka.


Lakini mbele ya kukata hamu yao, chakula kilipokuwa kingali katika kinywa,


Kuzimu na shimo la kuangamia havishibi hata kidogo, vilevile macho ya watu hayashibi.


Usimutamani mwanamuke yule kwa uzuri wake, wala usikubali kunaswa kwa kope za macho yake.


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Kwa hiyo pahali pale pakapewa jina Kibroti-Hatawa, ni kusema “Makaburi ya Hamu”, kwa sababu huko ndiko walikozika watu waliokuwa na hamu ya kula nyama.


Kati ya Waisraeli kulikuwa kundi fulani lililoandamana nao ambalo lilikuwa na hamu kubwa ya kula nyama. Waisraeli wenyewe wakalia, wakisema: Heri kama tungeweza kupata nyama ya kula!


Shetani akamupeleka tena mpaka juu ya mulima murefu, akamwonyesha falme zote za dunia na utajiri wao.


Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemwangalia mwanamuke kwa kumutamani, amekwisha kuzini naye ndani ya moyo wake.


Kisha Shetani akamupeleka kwenye nafasi inayoinuka juu sana. Akamwonyesha mara moja falme zote za dunia,


Lakini Bwana Yesu akuwe kama vile silaha munayobeba, musijiachilie kuvutwa na hali yenu ya kimwili hata mutimize tamaa zake.


Mambo hayo ni mufano kwetu, kusudi tusikuwe na tamaa mbaya kama vile wao.


Kwa maana tamaa za kimwili zinapingana na tamaa za Roho Mutakatifu. Na tamaa za Roho zinapingana na tamaa za kimwili. Hao wawili wanapingana hata munashindwa kufanya sawa vile munavyotaka.


Nao watu wa Kristo Yesu wameua hali yao ya kimutu pamoja na vifungo vyao vyote na tamaa zote mbaya.


Zamani, sisi wote vilevile tulikuwa kama wao. Tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kimwili na kutenda kufuatana na mapenzi ya mwili na roho zetu. Kwa sababu ya hali yetu ya kimwili, hatungeponyoka kasirani ya Mungu kama wengine.


Neema hii inatufundisha kwamba tuache uovu na tamaa za dunia, na kuishi katika dunia hii ya sasa katika ukadirifu, katika haki na kushikamana na ibada.


Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.


Hekima ya namna hii haitoki mbinguni; lakini ni ya dunia, nayo ni ya kimwili na ya kishetani.


Lakini sasa munajivuna na kujisifu. Majivuno yote ya namna hii ni mabaya.


Nilipoona vazi moja zuri kutoka Sinari kati ya vitu tulivyonyanganya, vikoroti mia mbili vya feza na furushi ya zahabu yenye uzito wa vikoroti makumi tano vya feza, nikavitamani na kuvitwaa; nikavificha katika udongo ndani ya hema langu; na feza iko chini ya vitu hivyo.”


Kama watoto wenye utii, musiachilie maisha yenu kutawaliwa na tamaa mbaya mulizokuwa nazo zamani wakati mulipokuwa mukiishi katika ujinga.


Wapendwa wangu, ninawasihi ninyi, kama vile wageni na wasafiri hapa katika dunia, muepuke tamaa za mwili zinazopigana na roho.


Na zaidi atawaazibu wale wanaoishi kufuatana na tamaa mbaya za kimwili na kuzarau mamlaka ya Mungu. Walimu wale wa uongo ni wenye kiburi, wenye kujivuna, nao hawaogopi kutukana viumbe vitukufu vya mbinguni.


Kwa maana kwa masemi yao ya kujivuna na yasiyokuwa na maana, na kwa njia ya tamaa zao mbaya za kimwili, wanawavuta watu ambao wanaanza kuwaepuka, na wale wanaoishi katika udanganyifu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ