Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 2:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Nimewaandikia ninyi watoto, kwa sababu mumemujua Baba. Ninawaandikia ninyi wababa, kwa sababu mumemujua yule aliyekuwa tangia mwanzo wa vitu vyote. Ninawaandikia ninyi vijana, kwa sababu muko na nguvu na Neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mumemushinda yule Mwovu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 2:14
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nimeshika neno lako ndani ya moyo wangu, kusudi nisikukosee.


Kama mukikaa ndani yangu na maneno yangu yanakaa ndani yenu, mutaomba chochote munachotaka, nanyi mutakipewa.


Ninyi hamuchungi neno lake ndani yenu, kwa sababu ninyi hamumwamini yule aliyetumwa naye.


Basi Yesu akawaambia wale Wayuda waliomwamini: “Kama mukitii mafundisho yangu, ninyi ni wanafunzi wangu hakika.


Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Abrahamu. Lakini munatafuta kuniua, kwa sababu munakataa kukubali mafundisho yangu.


Basi kwa kumaliza, musimame imara katika kuungana kwenu na Bwana kwa uwezo wa nguvu zake kubwa.


Ninaweza vyote kwa njia ya Kristo anayenitia nguvu.


Mungu atawatia nguvu kwa uwezo wake wenye utukufu, kusudi mupate kuvumilia kila kitu pasipo kuchoka. Basi kwa furaha,


Habari za Kristo zikae ndani yenu kwa uwingi. Mufundishane na mushauriane kwa hekima. Mumwimbie Mungu kwa moyo wenu wote na kumushukuru kwa zaburi na nyimbo za kiroho.


Basi wewe mwana wangu, ukuwe hodari kwa njia ya neema uliyopata katika kuungana kwako na Kristo Yesu.


Sasa hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa ufalme wa Israeli katika siku zile: nitawawezesha kuchunga sheria zangu ndani ya mafikiri yao, nikiziandika ndani ya mioyo yao. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.


Tunawaandikia ninyi juu ya Neno la uzima, lililokuwa tangia mwanzo. Sisi tulilisikia, tuliliona kwa macho yetu wenyewe, tuliliangalia na kuligusa kwa mikono yetu wenyewe.


Tukisema kwamba hatukutenda zambi, tunamugeuza Mungu kuwa mwongo, na ukweli wa neno lake si ndani yetu.


Ninawaandikia ninyi wababa, kwa sababu mumemujua yule aliyekuwa tangu mwanzo wa vitu vyote. Ninawaandikia ninyi vijana kwa sababu mumemushinda yule Mwovu.


kwa sababu ukweli huu unakaa ndani yetu nao utakuwa pamoja nasi hata milele.


Nilifurahi sana wakati wandugu wamoja walipofika na kunielezea juu ya ukweli unaokuwa ndani yako na kwamba unaishi katika ukweli.


Wewe ni muvumilivu; umeteswa kwa ajili ya jina langu, lakini haukuregea.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda nitamupa ruhusa ya kula matunda ya muti wa uzima unaokuwa katika bustani ya Mungu!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ