Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 1:7
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Umejifunika mwangaza kama kanzu, umekunjua mbingu kama hema;


Ee Mungu, nitatimiza ahadi zangu kwako; nitakutolea sadaka za shukrani,


Haki na sheria ndio musingi wa utawala wako; wema na uaminifu vinakutangulia!


Mwangaza unamwangazia mutu wa haki, nayo furaha ni kwa watu wenye moyo wa usawa.


Sasa, enyi wazao wa Yakobo, mukuje, tutembee katika mwangaza wa Yawe.


Hakuna atakayesema tena ni mugonjwa; watu watasamehewa uovu wao wote.


Naye akinigusa nalo kwenye mudomo, akasema: Kaa hili limekugusa kwenye mudomo; umeondolewa kosa lako, umesamehewa zambi yako.


Watu wawili wanaweza kusafiri pamoja bila kupatana kwanza?


Siku hiyo, kutatokea chemichemi ya kutakasa zambi na uchafu wa wazao wa Daudi na wakaaji wote wa Yerusalema.


Utusamehe makosa yetu, kama sisi tunavyowasamehe wanaotukosea,


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Yesu akawaambia: “Mwangaza ungali kati yenu kwa muda kidogo. Mutembee wakati mungali na mwangaza, kusudi giza lisiwafunike, kwa sababu anayetembea katika giza hajui pahali anapokwenda.


kwa sababu malaika wa Bwana alishuka mara kwa mara ndani ya kile kisima na kutikisa maji. Na mugonjwa wa kwanza aliyeingia ndani ya maji kisha kuyatikisa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.]


Usiku umepita, na muchana unakaribia. Basi tutupilie mbali matendo ya giza na kuvaa silaha za kupigana nazo wakati wa mwangaza.


Na wamoja kati yenu walikuwa kama wao. Lakini mumesafishwa toka zambi, mumetakaswa na kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.


Kwa njia ya damu ya Kristo, sisi tumekombolewa, maana yake zambi zetu zimesamehewa. Hivi Mungu ameonyesha uwingi wa neema yake


Zamani muliishi katika giza, lakini sasa, kwa kuungana kwenu na Bwana, munaishi katika mwangaza. Muishi kama watoto wa mwangaza,


Ni yeye tu asiyeweza kufa na anayekaa katika mwangaza ambao mutu hawezi kukaribia. Hakuna mutu aliyemwona wala hakuna mutu anayeweza kumwona. Ndiye mwenye heshima na uwezo wa milele! Amina.


Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.


Ikiwa ni hivi, damu ya Kristo haitakuwa na uwezo zaidi wa kututakasa? Kwa maana kwa njia ya Roho anayeishi kwa milele, Kristo alijitoa mwenyewe kwa Mungu kuwa sadaka kamilifu. Nayo damu yake ikazitakasa zamiri zetu toka katika matendo yasiyofaa, kusudi tupate kumutumikia Mungu Mwenye Uzima.


Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


Lakini mulikombolewa kwa njia ya damu yenye bei kali ya Kristo, aliyekuwa kama kondoo asiyekuwa na kilema wala uchafu.


Lile tuliloona na kulisikia, ndilo tunalotangaza kwenu vilevile, kusudi mupate kushirikiana nasi. Na huu ushirika wetu ni ule tunaokuwa nao pamoja na Baba na Mwana wake Yesu Kristo.


Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kutoka kwa Yesu Kristo na kuitangaza kwenu: Mungu ni mwangaza, na ndani yake hamuna giza hata kidogo.


Yesu Kristo ndiye aliyekuja kwa maji ya ubatizo wake na kwa damu ya kufa kwake. Hakukuja na maji tu, lakini pamoja na maji na damu. Naye Roho ndiye anayeshuhudia mambo yale kwa sababu Roho ni wa ukweli.


Roho, maji na damu, nao watatu wanapatana kwa ushuhuda mumoja.


Nilifurahi sana kuona kwamba wamoja kati ya watoto wako wanaishi katika ukweli kama vile Baba alivyotuamuru.


Hakuna jambo linalonifurahisha kuliko lile la kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.


na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.


Wandugu zetu wamemushinda kwa nguvu ya damu ya Mwana-Kondoo na kwa njia ya ukweli walioshuhudia. Wao walikubali kutoa maisha yao mpaka kufa.


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ