Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Uzima huu ulipotokea, sisi tuliuona. Kwa sababu hii tunaushuhudia na kuwatangazia habari za huo uzima wa milele, uliokuwa pamoja na Baba na ulioonyeshwa kwetu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 1:2
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


Yeye alikuwa chemichemi ya uzima, na uzima huu ulikuwa mwangaza kwa watu.


Mimi ninawapa uzima wa milele, nao hawatapotea hata milele, wala hakuna mutu anayeweza kuwanyanganya toka katika mukono wangu.


Yesu akamujibu: “Mimi ni njia, ukweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba asipopitia kwangu.


Na ninyi vilevile mutanishuhudia, kwa sababu mumekuwa pamoja nami tangu mwanzo.


Nilitoka kwa Baba, nami nimekuja katika dunia. Sasa ninaacha dunia na kurudi kwa Baba.”


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


Na sasa, Baba, unipe utukufu karibu nawe, utukufu unaokuwa sawa na ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuumbwa kwa dunia.


Mutu aliyeona mambo hayo ndiye anayeyashuhudia, nao ushuhuda wake ni wa kweli. Na anajua kama anasema ukweli, kusudi mupate kuamini vilevile.


Hii ndiyo mara ya tatu Yesu aliyowatokea wanafunzi wake tangu alipofufuka.


Na zaidi ya hii hakuna mutu aliyepanda mbinguni, isipokuwa Mwana wa Mutu aliyeshuka toka mbinguni.


lakini mimi ninamujua sababu nilitoka kwake, naye ndiye aliyenituma.”


Mimi ninasema yale niliyoona kwa Baba yangu, lakini ninyi munafanya yale muliyosikia kutoka kwa baba yenu.”


Hakuonekana kwa watu wote, lakini kwa sisi tuliochaguliwa na Mungu kuwa washuhuda. Ni sisi tuliokula na kunywa pamoja naye nyuma ya kufufuka kwake.


“Mungu alimufufua huyo Yesu, na sisi wote tuko washuhuda wa jambo hili.


Halafu mukamwua yule anayekuwa asili ya uzima, lakini Mungu amemufufua. Na sisi ni washuhuda wa jambo hilo.


Na sisi ni washuhuda wa mambo hayo, naye Roho Mutakatifu ambaye Mungu aliwapa wale wanaomutii, anayashuhudia vilevile.”


Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Lakini neema hii imeonekana sasa kwa kuja kwa Mwokozi wetu Kristo Yesu. Yeye ameshinda nguvu za lufu na kwa njia ya Habari Njema ameonyesha wazi uzima wa milele.


Na kwa njia hiyo watapata tumaini la uzima wa milele, ambalo Mungu asiyesema uongo alituahidi mbele ya mwanzo wa nyakati.


Ninawaonya wazee wa kanisa wanaokuwa kati yenu. Mimi vilevile ni muzee mwenzenu, nami ni mushuhuda wa mateso ya Kristo na zaidi ya hii nitashiriki katika utukufu ule utakaotokea.


Tunawaandikia ninyi juu ya Neno la uzima, lililokuwa tangia mwanzo. Sisi tulilisikia, tuliliona kwa macho yetu wenyewe, tuliliangalia na kuligusa kwa mikono yetu wenyewe.


Na Kristo yeye mwenyewe alituahidi sisi uzima wa milele.


Ninyi munajua kwamba Yesu Kristo alikuja kusudi aondoe zambi, na hakuna zambi ndani yake.


Mutu anayefanya zambi ni mutu wa Shetani, kwa maana Shetani anafanya zambi tangia mwanzo wa vitu vyote. Kwa sababu hii, Mwana wa Mungu alikuja kusudi aharibu kazi za Shetani.


Na sisi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemutuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa dunia.


Mutatambua Roho wa Mungu kwa njia hii: kila mutu anayesadiki kwamba Yesu Kristo amekuja katika hali ya kimutu yuko na Roho wa Mungu.


Na huu ndio ushuhuda ule: Mungu alitupatia uzima wa milele na uzima huu unapatikana kwa njia ya Mwana wake.


Ninawaandikia maneno yale, ninyi wenye kuamini kwa jina la Mwana wa Mungu, mupate kujua kwamba muko na uzima wa milele.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ