Lakini Wayuda wakawashawishi wakubwa wa muji pamoja na wanawake wamoja wenye heshima, walioabudu Mungu. Wakawatesa Paulo na Barnaba hata wakawafukuza toka katika inchi yao.
Na kulikuwa Mulawi mumoja muzaliwa wa kisanga cha Kipuro, jina lake Yosefu. Mitume walimwita kwa jina lingine la Barnaba, maana yake “Mwenye kutia moyo.”
Wandugu, munakumbuka namna tulivyosumbuka na kazi ngumu. Wakati tulipowahubiria Habari Njema ya Mungu, tulitumika muchana na usiku kusudi tusimulemee hata mutu mumoja kati yenu.