Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 9:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Au sina haki ya kusafiri pamoja na mwanamuke mukristo kama vile mitume wengine wanavyofanya, nao wandugu za Bwana na hata Petro?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 9:5
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Dada yangu, muchumba wangu, ni bustani yangu ya pekee, chemichemi inayochungwa.


Huyu si mwana wa yule seremala? Mama yake si Maria? Nao Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda si wandugu zake?


Kisha Yesu akafika kwa nyumba ya Petro, na mule akamukuta mama mukwe wa Petro amelala katika kitanda na ugonjwa wa homa.


Mama mukwe wa Simoni alikuwa katika kitanda, kwa sababu alikuwa na homa. Wakati Yesu alipofika pale, mara moja wakamupasha habari ya ugonjwa wake.


Huyu si yule museremala, mwana wa Maria, ndugu ya Yakobo, Yose, Yuda na Simoni? Nao wadada zake, si wanaishi hapa kati yetu?” Na kwa hiyo wakakosa kumwaminia.


Matayo na Toma, Yakobo mwana wa Alfayo na Simoni (wa kikundi cha Wazeloti),


Halafu watu wakamwambia Yesu: “Mama yako na wandugu zako wanasimama inje, wanataka kukuona.”


Kisha akamupeleka Simoni kwa Yesu. Yesu akamwangalia, akasema: “Wewe ndiwe Simoni mwana wa Yoane, sasa utaitwa Kefa.” (Jina “Kefa” ni sawasawa na “Petro” na maana yake ni “Jiwe.”)


Nyuma ya maneno yale, akaenda Kapernaumu pamoja na mama yake, wandugu zake na wanafunzi wake. Nao wakakaa kule siku chache.


Hawa wote walikuwa wakikusanyika kwa nia moja kwa kuomba, pamoja na wanawake wamoja, Maria mama wa Yesu, na wandugu za Yesu.


Ninawatumia dada yetu mwamini Foibe, anayekuwa musaidizi wa kanisa la Kenkurea.


Ninataka kusema: kila mumoja kati yenu anasema maneno yake mbalimbali. Mumoja anasema: “Mimi ni wa Paulo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Petro,” na mwingine anasema: “Mimi ni wa Kristo.”


Lakini kama mume au muke mupagani akitaka kuachana na mwamini aliyeoana naye, aachane naye. Katika mambo kama hayo, ndugu au dada mwamini yuko huru, kwa maana Mungu amewaita kusudi mukae katika amani.


Mwanamuke aliyeolewa anafungwa na Sheria katika maisha yake na mume wake wakati mume wake angali muzima. Lakini kama mume wake akikufa, yeye ni huru kuolewa na yule anayetaka, lakini sherti ndoa ikuwe ya kikristo.


Hakika, ningetamani watu wote wakuwe kama mimi, lakini kila mutu amepewa zawadi yake ya kipekee na Mungu, mumoja zawadi hii, na mwingine zawadi ile.


Na kwa wale wasiooa bado na wajane, ninawaambia kwamba ingekuwa vema waendelee kuishi peke yao kama vile mimi.


Sikumwona mutu mwingine isipokuwa tu Yakobo, ndugu ya Bwana.


Basi musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja tu, akuwe mukadirifu, mwenye akili, akuwe mwema na mwenye kupenda kukaribisha wageni na mwenye kujua kufundisha.


Wao wanafundisha kwamba ni vibaya kuoana, na wanawakataza watu kula vyakula fulani fulani. Lakini Mungu aliumba vyakula vile kusudi watu waliokwisha kumwamini na kutambua ukweli wapate kuvitumia wakisha kumushukuru.


nao wanawake wazee kama mama yako na vijana wanawake kama wadada zako, ukijilinda katika maisha safi.


muzee wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja nao watoto wake wanapaswa kuwa waamini na wasioshitakiwa neno juu ya mwenendo mubaya au juu ya kukosa utii.


Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ