Lakini kwa sababu waliongoza ibada za miungu kwa ajili ya watu wa Israeli, wakasukuma watu kutenda zambi, basi, nimeunyoosha mukono wangu kuwaazibu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Nao watabeba azabu yao.
“Mufanye angalisho, musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa sababu ninawaambia kwamba wamalaika wao wanaokuwa mbinguni wako siku zote karibu na Baba yangu anayekuwa mbinguni. [
Sisemi juu ya zamiri zenu, lakini juu ya zamiri ya yule aliyewaarifu. Labda kuna mutu anayeweza kuuliza: “Kwa sababu gani ninaweza kuzuizwa kutenda sawa na uhuru wangu kwa ajili ya mwingine?
Kwa maana kama mutu zaifu katika imani akikuona wewe mwenye elimu unakula katika hekalu la sanamu, si zamiri yake itamusukuma kula vyakula vya kutambikia sanamu?
Na kwa wale wanaokuwa zaifu katika imani, ninajifanya kama muzaifu kusudi niwapate hao wanaokuwa zaifu. Kwa wote nimejifunza kuwa mwenye hali kama yao, kusudi nipate kuokoa wamoja kati yao kwa njia mbalimbali.
Ninasikia haya ya kuisema: tumekuwa zaifu kwa kufanya vile! Lakini kama watu wengine wanasubutu kujivuna juu ya kitu chochote, mimi vilevile nitajivuna. Sasa ninasema kama vile mupumbafu.
Wandugu, ninyi muliitwa na Mungu kusudi mukuwe watu huru. Basi musitumie uhuru huu kuwa ruhusa ya kutimiza tamaa za mwili, lakini musaidiane kwa upendo.
Mujiangalie hata mutu asiwapotoshe kwa elimu yake ya udanganyifu mutupu inayotegemea desturi za watu na roho mbaya zinazotawala dunia, lakini haitegemei mafundisho ya Kristo.
Wanawaahidi watu wengine kwamba watakuwa huru ijapokuwa wao wenyewe ni watumwa wa upotovu. Kwa maana kila mutu ni mutumwa wa jambo lolote linalomutawala.
Lakini niko na neno hili juu yako: kati yako kuna watu wamoja wanaoshika mafundisho ya Balama. Huyu ndiye aliyemufundisha Balaka kwamba awapime Waisraeli, kusudi wakule vyakula vya kutambikia sanamu za miungu na kufanya uasherati.