Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 8:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Basi kuelekea lile ulizo juu ya kula nyama za kutambikiwa kwa sanamu za miungu, tunajua kwamba sanamu ni kitu bure katika dunia, na ya kuwa kuna Mungu mumoja peke yake tu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 8:4
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe ndiwe mukubwa, unafanya maajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.


“Ee Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, unayeikaa katika kiti cha kifalme juu ya makerubi, ni wewe tu unayekuwa Mungu, unayetawala falme zote za ulimwengu. Wewe uliumba dunia na mbingu.


Sasa, ee Yawe, Mungu wetu, utuokoe toka katika makucha ya Saniharibu, kusudi falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe peke yako, ee Yawe, ambaye ni Mungu.”


Hakika, ninyi si kitu kabisa. Hamuwezi kufanya kitu chochote. Anayechagua kuwaabudu ninyi ni chukizo.


Yawe, Mukombozi wako, aliyekuumba tangu katika tumbo, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe niliyeumba vitu vyote. Mimi peke yangu nilizitandaza mbingu, niliiumba dunia kwa nguvu yangu mwenyewe!


Yawe, Mufalme na Mukombozi wa Israeli, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mimi ni wa kwanza na wa mwisho; hakuna mungu mwingine isipokuwa mimi.


Yawe anasema hivi: Utajiri wa Misri na faida ya uchuuzi za Kushi, pamoja na za watu wa Seba, wale watu warefu sana, zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli, zote zitakuwa mali yako. Watu hao watakufuata wakifungwa minyororo; watainama mbele yako na kukusihi wakisema: Kwako kuna Mungu wa kweli, wala hakuna Mungu mwingine lakini yeye.


Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine; hakuna Mungu mwingine lakini mimi. Ninakuimarisha ingawa wewe haunijui,


Lakini Yawe ni Mungu wa kweli, Mungu Mwenye Uzima, mufalme wa milele. Akikasirika, dunia inatetemeka, mataifa hayawezi kuvumilia hasira yake.


Mwanadamu ni mujinga na mupumbafu; kila mufua zahabu anafezeheshwa na sanamu zake. Sanamu hizo ni uongo mutupu, hazina uzima wowote ndani yao.


Yesu akamujibu: “Amri ya kwanza katikati ya zote ni hii: ‘Sikia, wewe taifa la Waisraeli! Bwana Mungu wetu ndiye Bwana peke yake.


“Wandugu, kwa sababu gani munafanya mambo kama haya? Sisi vilevile ni watu, tuko sawasawa nanyi, na tunawahubiri ninyi Habari Njema kwamba muache kuabudu vitu hivi vya bure na mumugeukie Mungu mwenye uzima; yeye aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yao.


Lakini inafaa tuwaandikie kwa kuwaambia kwamba wajitenge na vitu vilivyochafuliwa kwa kutambikia sanamu, waepuke uasherati na wasikule nyamafu wala damu.


Sasa ninyi wenyewe munaona na kusikia namna huyu Paulo anayofanya. Amekwisha kuwavuta na kuwaonya watu wengi, si hapa Efeso tu, lakini ni karibu katika jimbo lote la Azia. Anasema kwamba miungu inayotengenezwa na watu si miungu hata kidogo.


Sasa tuangalie mambo yanayoelekea nyama zinazotolewa kwa kutambikia sanamu za miungu: tunajua kwamba “sisi wote tuko na elimu,” kama vile munavyozoea kusema. Elimu inamufanya mutu kuwa na kiburi, lakini upendo unawajenga watu katika imani.


Kwa maana kama mutu zaifu katika imani akikuona wewe mwenye elimu unakula katika hekalu la sanamu, si zamiri yake itamusukuma kula vyakula vya kutambikia sanamu?


Na hivi kwa sababu ya elimu yako, yule ndugu mwamini zaifu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, atapotea.


Zamani, mulipokuwa hamumujui Mungu, mulikuwa watumwa wa miungu isiyokuwa ya kweli.


Mungu mumoja, Baba ya watu wote, anayekuwa juu ya wote, anayetumika kwa njia ya wote, na anayekaa ndani ya wote.


‘Ee Bwana wetu Yawe, ninajua umenionyesha mimi mutumishi wako mwanzo tu wa ukubwa wako na uwezo wako. Maana, kuna mungu gani huko mbinguni au katika dunia anayeweza kufanya mambo makubwa na ya ajabu kama vile ulivyofanya wewe?


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Ninyi mulijaliwa kuona mambo hayo, kusudi mupate kutambua kwamba Yawe ndiye peke yake Mungu na wala hakuna mwingine.


Basi, mukumbuke leo na kuweka ndani ya mioyo yenu, kwamba Yawe ndiye Mungu juu mbinguni na chini katika dunia. Hakuna mwingine.


“Basi musikilize, enyi Waisraeli! Yawe, Yawe tu, ni Mungu wetu.


Kwa Mufalme wa milele, asiyeweza kufa, asiyeonekana, Mungu peke yake, ikuwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.


Kwa maana kuna Mungu mumoja tu, na kuna mupatanishi mumoja tu kati ya Mungu na watu, ni yule mutu, Kristo Yesu,


yeye anayekuwa Mungu peke yake, Mwokozi wetu, asifiwe na kuwa na ukubwa, uwezo na mamlaka, kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu, tangia zamani za kale, sasa na hata milele! Amina.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ