Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 8:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kwa kuwakosesha wandugu zenu kama hivi na kuumiza zamiri yao, ni kama vile munamukosea Kristo mwenyewe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 8:12
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo Abimeleki akamwita Abrahamu, akamwuliza: “Umetutendea nini? Nimekukosea nini hata ukaniletea zambi kubwa, mimi na ufalme wangu? Umenitendea mambo yasiyostahili kutendwa.”


Rubeni akawaambia: “Si niliwaambia tusimuzuru kijana? Lakini ninyi hamukunisikiliza! Sasa tunaazibiwa kwa ajili ya damu yake.”


Tena Musa akasema: “Magaribi, Yawe atawapa nyama mupate kula na asubui atawapa mikate mupate kula na kushiba. Maana yeye ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie? Musitunungunikie sisi lakini mumunungunikie Yawe.”


Musa akamwuliza Haruni: Walikufanya nini watu hawa hata ukawaingiza katika zambi kubwa hivyo?


“Mufanye angalisho, musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa sababu ninawaambia kwamba wamalaika wao wanaokuwa mbinguni wako siku zote karibu na Baba yangu anayekuwa mbinguni. [


Kisha Petro akamwendea Yesu na kumwuliza: “Bwana, ndugu yangu akiendelea kunikosea, nitamusamehe mpaka mara ngapi? Mara saba inatosha?”


“Lakini anayeangusha mumoja wa hawa wadogo wanaoniamini, ingalikuwa heri afungiwe jiwe kubwa la kusagia katika shingo na kuzamishwa ndani ya bahari.


Mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mumoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.’


Naye mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokosa kumutendea mumoja wa hawa wanaohesabiwa kuwa wadogo, hamukunitendea mimi.’


“Yeyote atakayeangusha mumoja wa hawa wadogo wanaoniamini, ingelikuwa heri afungiwe jiwe kubwa la kusagia katika shingo na kutupwa ndani ya bahari.


Ingekuwa heri afungiwe jiwe kubwa la kusagia katika shingo na kutumbukizwa ndani ya bahari, kuliko kumwangusha mumoja wa wadogo hawa.


Usiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya maneno ya chakula. Hakika vyakula vyote vinaruhusiwa kukuliwa, lakini ni vibaya kwa mutu kula chakula kinachoweza kukwaza mwingine.


Kwa maana, Kristo ni kama mwili mumoja unaokuwa na viungo vingi. Ijapokuwa viungo vya mwili ni vingi, vinakuwa mwili mumoja tu.


Mutu akimukosea mwenzake, anaweza kuombewa kwa Mungu, kusudi Mungu amusamehe. Lakini mutu akimukosea Yawe nani anayeweza kumwombea musamaha?” Lakini watoto hao hawakumusikiliza baba yao, maana Yawe alikwisha kata shauri la kuwaua.


Sasa, leo umejionea kwa macho yako mwenyewe. Ulipokuwa ndani ya pango Yawe alikutia katika mikono yangu. Wamoja kati ya watu wangu waliniambia nikuue, lakini nilikuhurumia. Nikasema sitanyoosha mukono wangu juu ya bwana wangu maana yeye ni muchaguliwa wa Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ