Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 7:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Yeye anashugulikia mambo mawili. Vilevile mwanamuke asiyeolewa au binti anashugulikia mambo ya Bwana. Anajitolea kwa Bwana katika mawazo na matendo yake yote. Lakini mwanamuke anayeolewa, anashugulikia mambo ya dunia, anatafuta jinsi ya kumupendeza mume wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 7:34
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye hashuguliki na kondoo kwa sababu anatumikia mushahara tu.


Musitoe tena viungo vya mwili wenu kufanya zambi, mukivitumikisha kama vyombo vya kufanya mabaya. Lakini mujitoe wenyewe kwa kumutumikia Mungu kama watu waliofufuliwa na mutumikishe viungo vya mwili wenu kama vyombo vya kufanya haki.


Kwa sababu mulinunuliwa na Mungu kwa bei kali. Basi mutumie miili yenu na roho zenu kwa utukufu wa Mungu.


Lakini mutu aliyeoa anasumbukia mambo ya dunia, anatafuta jinsi ya kupendeza muke wake.


Maneno hayo ninayosema ni kwa faida yenu, wala si kwa kuwafungia njia. Ninataka kuwaonyesha namna ya kuishi sawa inavyofaa, kusudi mupate kumutumikia Bwana pasipo kizuizo chochote.


Na bila kutaja mambo yote mengine kama hayo, kila siku ninashugulika na makanisa yote.


Shukrani kwa Mungu aliyemutia Tito bidii ya kuwasaidia kama vile sisi tunavyokuwa nayo!


Kwa maana kama vile ninavyongojea na kutumainia sana, sitafezeheka hata kidogo. Lakini tangia sasa na hata siku zote, nitamutukuza Kristo kwa uhodari katika maisha yangu, ikiwa nitaishi au nitakufa.


Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa, alinde uzima wenu wote ndiyo roho, moyo na mwili wenu, kusudi visikutiwe na kosa wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudia.


Kwa maana mutu anayeshindwa na kuongoza jamaa yake mwenyewe, namna gani ataweza kuchunga kanisa la Mungu?


Mujane wa kweli asiyekuwa na mutu yeyote wa kumusaidia, anamutumainia Mungu, na kudumu kumutolea mahitaji yake na kumwomba muchana na usiku.


Neno hilo ni la kuaminiwa. Ninataka uyatilie maneno hayo mukazo, kusudi watu walioamini Mungu wajitolee kwa kuzidi kutenda mema. Jambo hilo ni zuri na lenye mafaa kwa watu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ