Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 7:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Kwa maana mutumwa aliyeitwa kuwa wa Bwana, amepewa uhuru na Bwana. Hivi vilevile mutu mwenye uhuru aliyeitwa na Kristo, ni mutumwa wa Kristo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 7:22
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Yawe, mimi ni mutumishi wako, mutumishi wako, mutoto wa mujakazi wako. Umenifungulia vifungo vyangu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Kristo Yesu, niliyeitwa na Mungu kuwa mutume na niliyewekwa kwa kazi ya kutangaza Habari Njema yake.


Ikiwa ulikuwa mutumwa wakati Mungu alipokuita, usihuzunike. Lakini ikiwa kuna bahati ya kupata uhuru, usiipoteze bure.


Mimi si mutumwa wa mutu yeyote. Lakini nimejifanya kuwa mutumwa wa watu kusudi nipate wengi kati yao sawa inavyowezekana.


Vilevile ninapokuwa kati ya wasioishi chini ya Sheria ya Musa, ninaishi kama wao, bila kuangalia Sheria, kusudi niwapate. Hii si kusema kwamba mimi sishiki sheria ya Mungu, kwa maana mimi ni chini ya uongozi wa sheria ya Kristo.


Basi kusema vile inaonyesha kwamba ninatafuta watu wanikubali? Hapana! Ninataka kukubaliwa na Mungu. Au ninatafuta kuwapendeza watu? Kama ningekuwa ningali ninatafuta kuwapendeza watu, singekuwa mutumishi wa Kristo.


Kristo ametukomboa katika utumwa kusudi tukuwe huru kabisa. Basi, musimame imara wala musijitie tena katika vifungo vya utumwa.


Wandugu, ninyi muliitwa na Mungu kusudi mukuwe watu huru. Basi musitumie uhuru huu kuwa ruhusa ya kutimiza tamaa za mwili, lakini musaidiane kwa upendo.


Mwanainchi mwenzenu Epafra anawasalimia vilevile. Yeye ni mutumishi wa Yesu Kristo, hachoki kwa kuwaombea ninyi, kusudi musimame imara mukikomaa kiroho na kuwa tayari kwa kutimiza kabisa mapenzi ya Mungu.


Kwa sababu sasa yeye si kama vile mutumwa tu, lakini amekuwa bora zaidi kuliko mutumwa: yeye ni ndugu mupendwa. Mimi ninamupenda sana, nawe utamupenda zaidi sana, kwanza kama vile mutumwa, tena kama vile ndugu katika Bwana.


Muishi kama watu wanaokuwa na uhuru, lakini musitumie uhuru wenu kwa kufunika ubaya, lakini muishi kama watumwa wa Mungu.


Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yuda, mutumishi wa Yesu Kristo na ndugu wa Yakobo. Ninawaandikia ninyi mulioitwa na Mungu Baba na munaoishi katika upendo wake na kulindwa kwa ajili ya Yesu Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ