Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Lakini kwa ajili ya kuepuka uasherati inafaa kila mwanaume akuwe na muke wake wa pekee, na kila mwanamuke akuwe na mume wake wa pekee.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 7:2
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anayemupata muke amepata kizuri; ni zawadi kutoka kwa Yawe.


Nyumba na mali ni urizi mutu anaopata kwa babu zake, lakini muke mwenye akili anatoka kwa Yawe.


Munauliza: Mbona sasa hazikubali? Yawe hazikubali kwa sababu anajua wazi kwamba umeivunja ahadi yako kwa muke wa ujana wako. Umekosa uaminifu kwake ingawa uliahidi mbele ya Mungu kwamba ungekuwa mwaminifu kwake.


Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayeachana na muke wake, isipokuwa tu kwa sababu ya uzinzi, anamufanya muke yule kuwa muzinzi kama akiolewa tena. Na mutu anayemwoa yule muke aliyefukuzwa, anazini vilevile.


Muepuke uzinzi! Zambi ingine yoyote mutu anayofanya haigusi mwili wake, lakini yule anayefanya uzinzi anafanya zambi juu ya mwili wake mwenyewe.


Sasa tuangalie mambo yale muliyoniandikia. Ni vizuri mwanaume asioe.


Mume anapaswa kumutimizia muke wake mapaswa yake, na muke anapaswa kumutimizia mume wake mapaswa yake.


Lakini kama hawawezi kujizuiza wao wenyewe, basi waoane; kwa maana afazali kuoa kuliko kuwaka tamaa.


Hivi vilevile waume wanapaswa kupenda wake wao kama vile wanavyopenda miili yao wenyewe. Yule anayependa muke wake, anajipenda yeye mwenyewe.


Ingawa hivi, kwa ngambo yenu vilevile, kila mume anapaswa kumupenda muke wake kama vile anavyojipenda, na kila muke anapaswa kuheshimu mume wake.


Kila mwanaume anapaswa kujua namna ya kuishi na muke wake katika hali ya utakatifu na ya heshima,


Wao wanafundisha kwamba ni vibaya kuoana, na wanawakataza watu kula vyakula fulani fulani. Lakini Mungu aliumba vyakula vile kusudi watu waliokwisha kumwamini na kutambua ukweli wapate kuvitumia wakisha kumushukuru.


Baba zao au kaka zao wakikuja kutulalamikia tutawaambia: “Sisi tunawaomba muwahurumie watu wa Benjamina na kuwaacha watwae hao wanawake; maana hatukupata wanawake wa kutosha katika vita ya Yabesi-Gileadi. Na kwa sababu si ninyi wenyewe muliowapatia hao wabinti zenu, hamutahukumiwa kwamba mumevunja kiapo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ