Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 7:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Ikiwa mutu alitahiriwa mbele ya kuitwa na Mungu, asitafute kufuta kovu la kutahiriwa kwake. Ikiwa alikuwa hajatahiriwa wakati alipoitwa na Mungu, hapaswi kutahiriwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 7:18
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yakobo akaendelea kusema: “Ni kwa sababu hii, mimi ninaona kwamba haifai tuwasumbue watu wa mataifa mengine wanaomugeukia Mungu.


Tumesikia kwamba watu fulani waliotoka huku kwetu pasipo ruhusa yetu wamewasumbua ninyi na maneno na kuwatia katika wasiwasi.


Kwa maana kutokana na shauri la Roho Mutakatifu na shauri letu wenyewe tumeamua kwamba hatutawabebesha muzigo mwingine muzito kupita mapaswa haya ya lazima:


Lakini wanafunzi wamoja waliokuwa katika chama cha Wafarisayo wakasimama na kusema: “Sherti watu wa mataifa mengine walioamini watahiriwe na kuagizwa wafuate Sheria ya Musa.”


Lakini wamesikia habari juu yako kwamba unawafundisha Wayuda wote wanaokaa katika inchi za mataifa wasishike Sheria ya Musa. Umewakataza wasiwatahiri watoto wao wala kufuata desturi zetu za kiyuda.


Kwa hiyo hakuna tena tofauti kati ya watu wa mataifa mengine na Wayuda, wenye kutahiriwa na wasiotahiriwa, wageni, washenzi, watumwa na watu huru. Lakini Kristo ni yote naye yuko katika wote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ