Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 7:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kwa ngambo ingine, kila mutu aendelee kuishi kufuatana na zawadi aliyopewa na Bwana na kufuatana na vile alivyokuwa mbele ya kuitwa na Mungu. Hii ndiyo kanuni ninayofundisha katika makanisa yote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 7:17
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kulingana na hayo, watu wamoja hawawezi kuoa kwa sababu walizaliwa towashi, wengine wamefanywa kuwa towashi na watu, wengine wamejifanya vile wenyewe kwa sababu ya kutumikia Ufalme wa mbinguni. Anayeweza kukubali mafundisho haya, ayakubali!”


Basi muangalie, kusudi musiwakwaze Wayuda, wala wasiokuwa Wayuda, wala kanisa la Mungu.


Lakini kama mutu akitaka kubishana juu ya neno hili, ajue kwamba sisi wala makanisa ya Mungu hatuna desturi ingine.


Kama mutu akiwa na njaa, akule katika nyumba yake, kusudi musikusanyike kwa kujiletea azabu. Basi maneno mengine yanayobaki nitayatengeneza wakati nitakapofika kwenu.


kwa maana Mungu hataki sisi tuishi katika fujo, lakini katika amani. Sawa vile inavyokuwa desturi katika makanisa yote ya watu wa Mungu,


Sasa juu ya muchango unaofanyika kwa ajili ya watu watakatifu wa Mungu wanaokuwa Yerusalema; ninyi vilevile mufanye sawa vile nilivyoagiza makanisa ya Galatia.


Ni kwa sababu hii ninawatumia ninyi Timoteo. Yeye ni mwana wangu mupendwa na mwaminifu mbele ya Bwana. Atawakumbusha kanuni ninazofuata katika maisha yangu na Yesu Kristo, nami ninazofundisha fasi zote katika makanisa yote.


Ikiwa mutu alitahiriwa mbele ya kuitwa na Mungu, asitafute kufuta kovu la kutahiriwa kwake. Ikiwa alikuwa hajatahiriwa wakati alipoitwa na Mungu, hapaswi kutahiriwa.


Wandugu zangu, inafaa kila mutu akae katika ushirika wake na Mungu akibaki sawa alivyokuwa wakati alipoitwa naye.


Hakika, ningetamani watu wote wakuwe kama mimi, lakini kila mutu amepewa zawadi yake ya kipekee na Mungu, mumoja zawadi hii, na mwingine zawadi ile.


Na bila kutaja mambo yote mengine kama hayo, kila siku ninashugulika na makanisa yote.


Pamoja naye tunamutuma ndugu anayesifiwa na makanisa yote kwa ajili ya kazi yake ya kuhubiri Habari Njema.


Katika siku zile makanisa ya Yudea yalikuwa hayajaniona kwa uso,


Wandugu, mambo yale yale yaliyotokea makanisa ya Mungu ya Yudea yanayoungana na Yesu Kristo, ndiyo yaliyowatokea ninyi vilevile. Kwa maana ninyi muliteswa na wanainchi wenzenu kama vile wao walivyoteswa na wanainchi wenzao Wayuda.


Kufuatana na ile, sisi tunajivuna kwa ajili yenu katika makanisa ya Mungu kwa sababu ya uvumilivu wenu na imani munayokuwa nayo katika mateso na taabu munazopata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ