Na kwa wengine, mimi ninawaambia maneno haya, lakini hayatoki kwa Bwana: kama mume mwamini akiwa na muke asiyeamini, naye muke yule akikubali kuishi pamoja naye, asimufukuze.
Kwa maana, mume asiyeamini anapata ushirika na Mungu kwa njia ya kuungana kwake na muke wake. Vilevile muke asiyeamini anapata ushirika na Mungu kwa njia ya kuungana kwake na mume wake. Kama isingekuwa vile, watoto wao wangehesabiwa kama watoto wa wapagani, lakini kwa hakika wao ni watu wa Mungu.