Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayeachana na muke wake, isipokuwa tu kwa sababu ya uzinzi, anamufanya muke yule kuwa muzinzi kama akiolewa tena. Na mutu anayemwoa yule muke aliyefukuzwa, anazini vilevile.
Na kwa wengine, mimi ninawaambia maneno haya, lakini hayatoki kwa Bwana: kama mume mwamini akiwa na muke asiyeamini, naye muke yule akikubali kuishi pamoja naye, asimufukuze.
Lakini kama mume au muke mupagani akitaka kuachana na mwamini aliyeoana naye, aachane naye. Katika mambo kama hayo, ndugu au dada mwamini yuko huru, kwa maana Mungu amewaita kusudi mukae katika amani.
Kuelekea wale ambao hawajaoa wala kuolewa, sina neno la kuwaamuru kutoka kwa Bwana. Lakini nitawatolea shauri kufuatana na vile ninavyokuwa mutu anayestahili kuaminiwa, kutokana na neema niliyopewa na Bwana.