Anania akajibu: “Bwana, nimekwisha kusikia watu wengi wakisema habari za mutu huyo, wakieleza mabaya aliyowatendea watu wako watakatifu wanaokuwa Yerusalema.
Mutu yeyote asijidanganye mwenyewe. Kama mutu fulani kati yenu akijizania kuwa mwenye hekima ya kidunia, ajifanye kama mupumbafu kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.
Sisi ni wapumbafu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye hekima katika kuungana kwenu na Kristo. Sisi ni zaifu, lakini ninyi ni wenye nguvu. Tunazarauliwa, lakini ninyi munaheshimiwa!
Wakati mutu mumoja kati yenu anapokuwa na ugomvi na ndugu mwenzake mwamini, atasubutu namna gani kwenda kumushitaki mbele ya waamuzi wapagani pahali pa kumushitaki mbele ya watu wa Mungu?