Ee Yawe, mukono wako uwafukuze kati ya watu, tukio lao likuwe kutengana na wanaokuwa wazima. Uwashibishe kwa akiba uliyowawekea, watoto wao nao washibe na kuacha sehemu, wawaachie hata na wajukuu wao.
“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!
“Mujilinde vizuri, kusudi musilemewe na kutafuta kula ulafi, kulewa na kusumbukia maisha. Kama si vile, Siku ile ya kurudia kwa Kristo itawafikia kwa rafla
Na mbegu zilizoanguka katika miiba ni mufano wa wale wanaosikia, lakini masumbuko, utajiri na raha ya dunia vinawasonga hata wanashindwa kutoa matunda yanayokomaa.
Munajua hakika kwamba mukijitoa wenyewe kwa mutu fulani kuwa watumwa wake na kulazimishwa kumutii, munakuwa kweli watumwa wa yule munayemutii. Ikiwa ni utumwa wa zambi, mwisho wake ni kifo; ikiwa ni kumutii Mungu, mwisho wake ni maisha ya haki.
Munajua kwamba miili yenu ni viungo vya mwili wa Kristo. Basi nitatwaa kiungo cha mwili wa Kristo kwa kukifanya kuwa kiungo cha kahaba? Hapana hata kidogo!
Au hamujui kwamba mutu yule anayeungana na kahaba amekwisha kuwa mwili mumoja naye? Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Hao wawili watakuwa mwili mumoja.”
Kwa maana Mungu hakuwahurumia wale wamalaika waliofanya zambi, lakini aliwatupa katika jehenamu. Wao wanalindwa mule wakifungwa minyororo katika giza nzito wakingojea Siku ile ya hukumu.
Mukumbuke vilevile wamalaika wale waliokosa kulinda vema cheo chao, lakini wakaacha makao yao: Mungu akawaweka katika nafasi ya giza, wakifungwa minyororo ya milele kwa kungojea Siku ile ya hukumu.