Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 5:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kwa hiyo tufanye karamu yetu ya Pasaka pasipo kutumia mikate iliyotiwa chachu; ni kusema pasipo zambi na uovu. Lakini tutumie mikate isiyotiwa chachu; ni kusema katika usafi na ukweli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 5:8
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Heri mutu ambaye Yawe hamuhesabii kosa, mutu ambaye hana udanganyifu ndani ya moyo wake.


Machozi ni chakula changu muchana na usiku; ninaambiwa kila siku: “Mungu wako yuko wapi?”


Yawe akaendelea kusema: “Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu. Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mutaondoa chachu katika nyumba zenu. Mutu yeyote akikula kitu kilichotiwa chachu katika muda ule wa siku saba, anapaswa kuondolewa kati ya Waisraeli.


Katika siku hizo saba, musikuwe na chachu yoyote katika nyumba zenu. Mutu yeyote, akuwe mugeni au mwenyeji, akikula kitu kilichotiwa chachu, ataondolewa katika kusanyiko la Waisraeli.


Watakula nyama hiyo usiku uleule kisha kuichoma. Wataikula pamoja na mukate usiotiwa chachu na mboga chungu za majani.


Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu, na katika siku ya saba mutafanya sikukuu kwa heshima ya Yawe.


Kwa muda ule wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu. Kusikuwe mikate iliyotiwa chachu, wala chachu yoyote kati yenu na katika inchi yenu yote.


Juu ya mulima Sayuni, Yawe wa majeshi atawafanyia watu wote karamu ya nyama zenye kunona na divai nzuri, nyama tamu zenye mafuta, pamoja na divai safi.


Lakini ninyi watu wa Yerusalema mutaimba kwa furaha kama munavyofanya wakati wa makesha ya sikukuu. Mutajaa furaha kama watu wanaotembea kwa mudundo wa muziki wa filimbi kwenda kwenye mulima kwa Yawe, kikingio cha Israeli.


Siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo, sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu itaanza. Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu.


Halafu wanafunzi wakafahamu kwamba Yesu hakuwaambia kwamba wafanye angalisho na chachu ya mikate, lakini na mafundisho ya Wafarisayo na Wasadukayo.


Yesu akawaambia: “Muangalie vizuri, mujiepushe na chachu ya Wafarisayo na Wasadukayo.”


Yesu akawaagiza: “Mujiangalie vizuri, mujiepushe na chachu ya Wafarisayo na ya Herode.”


Wakati ule ule makundi mengi ya maelfu ya watu walikusanyika hata wakakanyaganakanyagana. Yesu akaanza kwanza kusema na wanafunzi wake, akiwaambia: “Mufanye angalisho na chachu ya Wafarisayo, maana yake unafiki wao.


Wakati Yesu alipomwona Natanaeli akikuja kwake akasema hivi juu yake: “Angalia Mwisraeli wa kweli asiyekuwa na udanganyifu ndani yake hata kidogo!”


kwa sababu mungali munatawaliwa na mambo ya kidunia. Kwa maana ikiwa kungali wivu na ugomvi katikati yenu, haionyeshi kwamba munatawaliwa na mambo ya kidunia, nanyi munaishi kufuatana na hali ya kimutu?


Habari inasikilika fasi zote kwamba kunafanyika uzinzi katikati yenu. Wanaeleza kwamba uzinzi huu ni ubaya mukubwa, usiofanyika hata katikati ya wapagani, kwa maana wanasema kwamba kuna mumoja wenu ambaye amekamata muke wa baba yake kuwa muke wake!


Hamuna kitu cha kujivunia! Hamujui vizuri mufano unaosema kwamba chachu kidogo inachachisha donge zima?


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Basi sisi si kama wengine wengi wanaochuuza neno la Mungu; lakini kwa sababu Mungu ndiye aliyetutuma, sisi tunasema ukweli mbele yake, kama vile watumishi wa Kristo.


Sisemi hivi kwa kuwaamuru, lakini kwa njia ya kuwaelezea habari za bidii ya wengine, ninataka kuwapima kusudi upendo wenu upate kutambulikana kuwa wa kweli.


Ninawatakia neema wale wote wanaomupenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usiokuwa na mwisho.


“Wanaume wote wa taifa lenu watakuja mbele ya Yawe, Mungu wenu, mara tatu kila mwaka, pahali ambapo Yawe, Mungu wenu atachagua: wakati wa sikukuu ya Pasaka, sikukuu ya kuvuna na wakati wa sikukuu ya vibanda. Wasitokee mbele ya Yawe mikono mitupu.


Musikule sadaka hiyo na mikate iliyotiwa chachu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu, nayo ni mikate ya mateso – kwa sababu mulitoka Misri kwa haraka; kwa hiyo, muda wote mutakaoishi mutakumbuka ile siku mulipotoka Misri.


“Sasa, basi, mumutii Yawe na kumutumikia kwa moyo wa haki na uaminifu. Muache kabisa miungu ile ambayo wazee wenu waliiabudu ngambo ya muto Furati na katika inchi ya Misri. Mumutumikie Yawe.


Sasa, musiishi tena kufuatana na tamaa za kimutu, lakini muishi kufuatana na mapenzi ya Mungu kwa muda unaowabakilia kwa kukaa katika dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ