Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 5:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Basi mujitakase, mukiondoa ile chachu ya zamani ya zambi. Hivi mutakuwa kama donge jipya, lisilotiwa chachu, sawa vile munavyokuwa kwa kweli. Mufanye vile kwa maana Kristo amekwisha kutolewa sadaka kwa ajili yetu kama vile kondoo wa Pasaka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 5:7
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akaendelea kusema: “Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu. Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mutaondoa chachu katika nyumba zenu. Mutu yeyote akikula kitu kilichotiwa chachu katika muda ule wa siku saba, anapaswa kuondolewa kati ya Waisraeli.


Yesu akawaambia tena mufano mwingine, akisema: “Ufalme wa mbinguni unafanana na chachu mwanamuke mumoja aliyoitwaa na kuichanga na vipimo vitatu vya unga kwa kuponda mikate hata yote ikapata kuvimba.”


Siku ya kwanza ya karamu ya sikukuu ya Mukate Usiyotiwa Chachu, wakati ambapo walichinja kondoo wa Pasaka, wanafunzi wa Yesu wakamwuliza: “Unataka tuende wapi kukutayarishia karamu ya Pasaka?”


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Wakati alipomwona Yesu akipita, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu.”


Siku ile ilikuwa siku ya matayarisho ya Pasaka, karibu na saa sita. Pilato akawaambia Wayuda: “Mufalme wenu huyu!”


Kristo alitolewa na Mungu kuwa sadaka ya usamehe wa zambi kwa njia ya damu yake kwa ajili ya wenye kumwamini. Mungu alifanya hivi kwa kuonyesha haki yake. Zamani, katika uvumilivu wake, aliacha kuazibu zambi za watu. Lakini kwa wakati wa sasa anaonyesha haki yake kusudi akuwe mwenye haki na kumuhesabia haki kila mutu anayemwamini Yesu.


Kwa kuwa mukate ni mumoja, ijapokuwa sisi ni wengi, tuko mwili mumoja, kwa maana sisi wote tunashiriki mukate ule mumoja.


Basi munapaswa kutupilia mbali ile hali yenu ya zamani, ule utu wenu wa zamani unaopotoka kufuatana na tamaa zake za udanganyifu.


Nao waliimba hivi kwa sauti kubwa: “Mwana-Kondoo aliyeuawa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima na nguvu, heshima, utukufu na sifa!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ