Wakati uliposikia niliyosema juu ya pahali hapa na juu ya wakaaji wake, kwamba watakuwa ukiwa na kulaaniwa, ulijuta na kunyenyekea mbele yangu, hata ukapasua nguo yako na kulia mbele yangu. Basi, nami vilevile nimekusikia.
Na kama musiponisikiliza, moyo wangu utalia machozi kwenye uficho, kwa sababu ya kiburi chenu. Nitalia kwa uchungu na kutoa machozi, maana watu wa Yawe wanapelekwa katika uhamisho.
akamwambia hivi: Pita katikati ya Yerusalema, upate kutia kitambulisho kwenye vipaji vya nyuso za watu wanaohuzunika na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika muji huu.
Muwaue wazee palepale, vijana wanaume na wabinti, watoto na wanawake; lakini kila mumoja mwenye kuwa na kitambulisho, musimuguse. Muanzie katika hekalu langu. Basi, wakaanza na wazee waliokuwa mbele ya nyumba ya Yawe.
Wakati huohuo mutu mumoja akamuleta mwanamuke mumoja Mumidiani katika nyumba yake, Musa na Waisraeli wote pamoja wakiwa wanaomboleza kwenye mulango wa hema la mukutano.
Kwa maana ninaogopa kwamba wakati ninapokuja kwenu, sitawakuta sawa vile ninavyotaka, nanyi hamutanikuta sawa vile munavyotaka. Ninaogopa kuwakuta katika fitina, wivu, kasirani, ugomvi, masingiziano, matetano, majivuno na fujo.
Ninaogopa kwamba kwa safari yangu ingine, Mungu wangu atanifanya tena kuwa mwenye haya mbele yenu. Nami nitalia kwa ajili ya watu wengi waliofanya zambi zamani nao hawakugeuka toka katika uasherati, uzinzi na tamaa mbaya walizofanya.