Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 5:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Habari inasikilika fasi zote kwamba kunafanyika uzinzi katikati yenu. Wanaeleza kwamba uzinzi huu ni ubaya mukubwa, usiofanyika hata katikati ya wapagani, kwa maana wanasema kwamba kuna mumoja wenu ambaye amekamata muke wa baba yake kuwa muke wake!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 5:1
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Israeli alipokuwa anakaa katika inchi ile, mwana wake Rubeni, akalala na Biliha, habara ya baba yake. Naye Israeli akasikia habari hizo. Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili.


Hizi ndizo habari za ukoo wa Yakobo. Yosefu, akiwa kijana wa umri wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo na mbuzi pamoja na wandugu zake, wana wa Biliha na Zilpa, wake za baba yake. Yosefu akakuwa anamujulisha baba yake juu ya tabia mbaya za wandugu zake.


Wewe ni kama maji ya mafuriko. Lakini hautakuwa wa kwanza tena, maana ulipanda juu ya kitanda changu mimi baba yako, wewe ulikichafua; hakika wewe ulipanda juu yake!


Kwa hiyo, watu wakamupigia Abusaloma hema kwenye paa, naye akalala na wahabara za baba yake, watu wote wa Israeli wakiwa wanaona.


Nyuma, Daudi alifika katika nyumba yake kule Yerusalema. Mufalme aliwatwaa wahabara wake kumi ambao alikuwa amewaacha kwa kuangalia nyumba yake, akawaweka kwenye nyumba moja wapate kulindwa, akawatunza vizuri, lakini hakulala nao. Kwa hiyo wahabara hao wakakuwa wakifungwa mpaka siku za kufa kwao, wakaishi kama vile walikuwa wajane.


Hawa ndio wazao wa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli. (Ingawa Rubeni alikuwa muzaliwa wa kwanza haki yake ya muzaliwa wa kwanza ilipewa kwa ndugu yake Yosefu kwa sababu Rubeni alilala na habara wa baba yake. Kwa hiyo, yeye hakutiwa katika hesabu ya ukoo kulingana na haki yake ya muzaliwa wa kwanza.


Kweli wewe ni bingwa wa kutafuta wapenzi! Hata wanawake waovu unawafundisha njia zako.


Lakini wewe haukutosheka kufuata mienendo yao au kutenda sawa na machukizo yao. Kwa muda mufupi tu ulipotoka kuliko vile wao walivyopotoka katika mienendo yako yote.


Kwako kuna watu ambao wanalala na wake wa baba zao. Wanalala kwa kinguvu na wanawake katika siku zao za ugonjwa wa mwezi.


Usimuvunjie heshima baba yako kwa kulala na mumoja wa wake zake. Hao ni wamama zako.


Mwanaume akilala na mumoja wa wake za baba yake, anamupatisha baba yake haya, wote wawili wanapaswa kuuawa. Mwanaume huyo na mwanamuke huyo wote wawili watauawa na damu yao itakuwa juu yao wenyewe.


Wanagandamiza wazaifu, na kuwabagua wamasikini wasipate haki zao. Mutoto na baba yake wanalala na binti mujakazi mumoja, hivyo wanalichafua jina langu takatifu.


Lakini inafaa tuwaandikie kwa kuwaambia kwamba wajitenge na vitu vilivyochafuliwa kwa kutambikia sanamu, waepuke uasherati na wasikule nyamafu wala damu.


musikule vyakula vilivyotolewa kwa kutambikia sanamu; musikule damu wala nyamafu; na muepuke uasherati. Mutafanya vema kama mukijitenga na mambo haya. Salamu kwenu.”


Kwa maana, wandugu zangu, nimepata habari zenu kwa njia ya jamaa ya Kloe kwamba kuko ugomvi katikati yenu.


Lakini niliwaandikia kwamba musishirikiane na mutu anayejiita ndugu mwamini, akiwa mwasherati, mwenye tamaa, mwenye kuabudu sanamu, mutukanaji, mulevi au munyanganyi. Na zaidi ya ile musichangie chakula na mutu wa namna hii.


Nanyi munasema vilevile: “Chakula kiliumbwa kwa ajili ya tumbo nayo tumbo kwa ajili ya chakula.” Ndiyo, lakini Mungu ataharibu vyote viwili. Lakini mwili haukuumbwa kwa ajili ya uasherati. Mwili uliumbwa kwa ajili ya Bwana nao ni wake.


Muepuke uzinzi! Zambi ingine yoyote mutu anayofanya haigusi mwili wake, lakini yule anayefanya uzinzi anafanya zambi juu ya mwili wake mwenyewe.


Ninyi munajua hakika kwamba watenda mabaya hawatapata urizi katika Ufalme wa Mungu. Musidanganyike: waasherati, wenye kuabudu sanamu, wazinzi, waasherati wa muke kwa muke na mume kwa mume,


Ninaogopa kwamba kwa safari yangu ingine, Mungu wangu atanifanya tena kuwa mwenye haya mbele yenu. Nami nitalia kwa ajili ya watu wengi waliofanya zambi zamani nao hawakugeuka toka katika uasherati, uzinzi na tamaa mbaya walizofanya.


Kulikuwa mutu aliyefanya mambo ya kuhuzunisha, hakunihuzunisha mimi, lakini amewahuzunisha ninyi wote au bila kwenda mbali zaidi wamoja kati yenu.


Basi ikiwa nimewaandikia, si kwa ajili ya yule aliyefanya kosa au si kwa ajili ya yule aliyemukosea. Lakini kusudi mupate kutambua waziwazi mbele ya Mungu bidii munayokuwa nayo kwa ajili yetu.


Matendo ya kimwili yanajulikana wazi, nayo ndiyo uasherati, uchafu, kutawaliwa na tamaa za kimwili,


Kama vile inavyowapasa watu wa Mungu kuishi, tendo lolote la uasherati, la uchafu wala la tamaa ya mali lisisikilike kati yenu.


“ ‘Alaaniwe mwanaume anayelala na muke wa baba yake, maana amemupatisha baba yake haya’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


Basi mutupilie mbali mambo yote ya kidunia yanayokuwa ndani yenu: uasherati, uchafu, nia mbaya, tamaa mbaya na tamaa ya mali inayokuwa sawa vile kuabudu sanamu.


Kwa maana Mungu hakutuita kusudi tuishi katika uchafu, lakini katika utakatifu.


Nimemwachia wakati wa kugeuka toka zambi zake, lakini hataki kuacha uasherati wake.


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


Musifanye hivyo wana wangu, kwa sababu mambo hayo ninayoyasikia kutoka kwa watu wa Yawe ni mabaya.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ