Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Sasa mumekwisha kupata vyote munavyohitaji! Mumekwisha kuwa watajiri! Munakuwa wafalme ingawa sisi hatuko wafalme. Heri mungekuwa kweli watawala kusudi nasi vilevile tupate kutawala pamoja nanyi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 4:8
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kuna mutu anayejidai kuwa tajiri, kumbe hana kitu. Mwengine anajiona kuwa masikini wakati ana mali tele.


Kama vile mawingu na upepo bila mvua, ndivyo anavyokuwa mutu anayeahidi zawadi na haitoi.


Ole kwao wanaojiona kuwa wenye hekima na akili.


Ikuwe hivyo! Yawe afanye hivyo. Yawe ayatimize maneno uliyotabiri, avirudishe hapa vyombo vya nyumba ya Yawe kutoka Babeli pamoja na watu wote waliohamishiwa huko.


Lakini Musa akamujibu: Unaona wivu kwa ajili yangu? Heri Yawe angewapa watu wake wote roho yake nao wapate kuwa manabii!


Yesu alipoona yale makundi ya watu, alipanda kwenye kilima. Alipokwisha kuikaa, wanafunzi wake wakamujongelea.


Ole kwenu ninyi munaoshiba sasa, maana mutasikia njaa. Ole kwenu ninyi munaocheka sasa, maana mutahuzunika na kulia.


Paulo akajibu: “Ikiwa wakati kidogo au wakati murefu, ninamwomba Mungu, si juu yako wewe mwenyewe tu, lakini hata hawa wote wanaonisikiliza leo wapate kuwa sawa mimi, lakini wasifikie tu kutiwa katika kifungo!”


Kufuatana na neema niliyopewa na Mungu, ninawaambia ninyi wote: mutu asijiwazie kuwa na ukubwa kupita vile inavyomustahili. Lakini mukuwe na mawazo ya ukadirifu, kila mumoja kulingana na kipimo cha imani aliyopewa na Mungu.


Kwa maana katika kuungana kwenu na Kristo, mumejaliwa katika vitu vyote, zaidi sana katika mambo yanayoelekea masemi na ufahamu.


Watu wamoja kati yenu wanajivuna wakifikiri kwamba sitakuja kuwaona.


Hamuna kitu cha kujivunia! Hamujui vizuri mufano unaosema kwamba chachu kidogo inachachisha donge zima?


Ingekuwa heri muvumilie kidogo masemi yangu ya upumbafu! Ninawaomba kweli munivumilie!


Tunafurahi wakati ninyi munapokuwa na nguvu, hata ikiwa sisi ni zaifu. Nasi tunawaombea kusudi mupate kuwa wakamilifu.


Kama mutu akijizania kwamba yeye ni kitu, ijapokuwa yeye si kitu, anajidanganya yeye mwenyewe.


Kitu cha lazima ni kwamba mukuwe na mwenendo unaolingana na mafundisho ya Habari Njema ya Kristo. Kwa hivi hata kama nikikuja kuwaona au hata kama nisipokuja, nipate tu kusikia kwamba munasimama imara katika nia moja, na kwamba wote pamoja munapigana vita kwa ajili ya imani inayotokana na Habari Njema.


Basi wapendwa wangu, mulionyesha utii wenu siku zote wakati nilipokuwa kwenu, na sasa ingekuwa vema muendelee kufanya vile katika siku hizi ninapokuwa mbali nanyi. Mutumike kwa ajili ya wokovu wenu kwa woga na kutetemeka,


Wewe unajidai kwamba uko tajiri mwenye mali mengi, wala haukosewi kitu. Lakini haujui kwamba wewe ni mukosefu, mwenye taabu, masikini, kipofu na mwenye kuwa uchi.


Umewapatia ufalme wa kikuhani kusudi wamutumikie Mungu wetu; nao watatawala katika dunia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ