Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 4:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Kweli zamiri yangu hainihukumu juu ya neno lolote, lakini hii si kusema kwamba mimi ni mwenye haki. Bwana ndiye anayenihukumu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 4:4
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutu ni nini hata aweze kuwa na moyo safi? Yule aliyezaliwa na mwanamuke atapata kuwa mwenye haki?


Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi?


Ninashikilia haki yangu, wala sitaiacha; katika zamiri yangu sina cha kunihukumu katika maisha yangu.


Mimi sifai kitu. Nitakujibu nini? Ninafunga kinywa changu.


Ingawa sina kosa, maneno yangu yenyewe yangenihukumu. Ingawa mimi ni mukamilifu, yangehakikisha kwamba mimi ni mupotovu.


Ee Yawe, kama ungekumbuka maovu yetu, nani, ee Bwana wetu, angeweza kuishi?


Usinitie katika hukumu mimi mutumishi wako, maana hakuna yeyote anayekuwa mwenye haki mbele yako.


Yananifundisha mimi mutumishi wako; kuyafuata kunaniletea zawadi kubwa.


Mimi nimesimama pahali penye kuwa imara; nitamusifu Yawe katika kusanyiko kubwa.


Mbingu zinatangaza haki ya Mungu; Mungu mwenyewe ndiye mwamuzi.


Matendo yote ya mutu ni sawa katika macho yake, lakini Yawe anapima mioyo.


Wengi wanapenda kujipendekeza kwa mutawala, lakini mutu anapata haki yake kwa Yawe.


Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.


Paulo akawakazia macho wale washauri wa Baraza Kubwa na kusema: “Wandugu zangu, mpaka leo zamiri yangu hainihukumu juu ya kitu chochote kinachoelekea mwenendo wangu mbele ya Mungu.”


Ni vile kwa sababu si wale wanaosikia Sheria ndio wanaohesabiwa haki mbele ya Mungu, lakini ni wale wanaotii Sheria.


Ikiwa Abrahamu alihesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya matendo yake, angeweza kujivuna. Lakini hawezi kujivuna mbele ya Mungu.


Kwa ngambo yangu, si neno hata kidogo kuhukumiwa nanyi au na tribinali ya watu. Na hata mimi mwenyewe sijihukumu.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Kwa maana sisi wote tunapaswa kusimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Kristo, kusudi kila mutu alipwe kufuatana na matendo yake mema au mabaya aliyofanya alipokuwa akiishi ndani ya mwili wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ