Mimi sisikii haya juu ya Habari Njema, kwa sababu huo ndio uwezo wa Mungu unaowaokoa wote wanaoamini, kwanza Wayuda na kisha watu wa mataifa mengine vilevile.
Kwa maana kazi ya Ufalme wa Mungu si kushugulika na mambo ya kula na kunywa, lakini ni kushugulika na haki, amani na furaha vinavyotolewa na Roho Mutakatifu.
kwa njia ya uwezo wa vitambulisho na maajabu, na kwa uwezo wa Roho Mutakatifu. Hivi tokea Yerusalema mpaka kufika katika jimbo la Iliriko nimehubiri fasi zote Habari Njema ya Kristo.
Kwa maana sioni haya hata kama nimejivuna zaidi kwa ajili ya uwezo Bwana aliotupatia sisi. Kwa maana uwezo ule ni kwa ajili ya kuwajenga katika imani, lakini si wa kubomoa.
Kwa maana tulipohubiri Habari Njema kwenu, hatukuihubiri kwa maneno tu, lakini kwa uwezo na kwa musaada wa Roho Mutakatifu na kwa uhakika kabisa. Munajua namna gani tulivyoishi katikati yenu, kusudi tupate kuwafalia.