Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yanayohitajika kwa mwenye madaraka kama hayo, ni kuwa mwaminifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 4:2
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zote zilitumiwa kwa kuwalipa wafanyakazi waliozitumia kwa kutengeneza nyumba ya Yawe.


Watu wanaosimamia ujenzi wasiombwe kutoa hesabu ya matumizi ya feza watakazopewa, kwa sababu wanazitumia kwa uaminifu.”


Mujumbe mubaya anawatumbukiza watu katika taabu, lakini mujumbe mwaminifu analeta amani.


Lakini juu ya mutumishi wangu Musa, hali ni tofauti kabisa. Yeye ana madaraka ya kuwatunza watu wangu wote.


Bwana wake akamwambia: ‘Ni vizuri, wewe mutumishi mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu katika ulinzi wa mali ndogo, basi nitakuweka kuwa mulinzi wa mali mengi. Kuja ufurahi pamoja na bwana wako.’


Bwana wake akamwambia: ‘Ni vizuri, wewe mutumishi mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu katika ulinzi wa mali ndogo, basi nitakuweka kuwa mulinzi wa mali mingi. Kuja ufurahi pamoja na bwana wako!’


Bwana akajibu: “Ni nani basi anayekuwa musimamizi mwaminifu na mwenye akili? Ni yule bwana wake aliyemuweka kwa kuwasimamia watumishi wake wengine na kumwamuru kuwapatia posho lao kwa wakati uliopangwa.


Kwa hiyo mutuhesabu kama watumishi wa Kristo, wanaoshugulika na ujumbe wa siri wa Mungu.


Ni kwa sababu hii ninawatumia ninyi Timoteo. Yeye ni mwana wangu mupendwa na mwaminifu mbele ya Bwana. Atawakumbusha kanuni ninazofuata katika maisha yangu na Yesu Kristo, nami ninazofundisha fasi zote katika makanisa yote.


Kwa ngambo yangu, si neno hata kidogo kuhukumiwa nanyi au na tribinali ya watu. Na hata mimi mwenyewe sijihukumu.


Kuelekea wale ambao hawajaoa wala kuolewa, sina neno la kuwaamuru kutoka kwa Bwana. Lakini nitawatolea shauri kufuatana na vile ninavyokuwa mutu anayestahili kuaminiwa, kutokana na neema niliyopewa na Bwana.


Basi sisi si kama wengine wengi wanaochuuza neno la Mungu; lakini kwa sababu Mungu ndiye aliyetutuma, sisi tunasema ukweli mbele yake, kama vile watumishi wa Kristo.


Tumekataa mambo ya kisirisiri na ya haya. Hatuna mwenendo wa udanganyifu wala hatupotowi neno la Mungu. Lakini tunajulisha waziwazi ukweli kusudi tuvute kila mutu kutuaminia katika zamiri yake mbele ya Mungu.


Ni Epafra mutumishi mwenzetu mupenzi, ndiye aliyewafundisha ninyi habari zile. Yeye ni mutumishi mwaminifu wa Kristo kwa ajili yetu.


Mumwambie Arkipo aangalie vizuri atimize kazi ile aliyopewa na Bwana.


Ndugu yetu mupendwa Tikiko mutumishi mwaminifu, na mwenzangu tunayetumika naye kazi ya Bwana atawapasha ninyi habari zangu zote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ