Lakini, ukimwonya mutu wa haki asitende zambi, naye akiacha kutenda zambi, hakika mutu huyo ataishi, kwa sababu amepokea maonyo yako, nawe utakuwa umeyaokoa maisha yako.
Hivi kuelekea maisha yenu na Kristo, hata mukiwa na walezi maelfu muko tu na baba mumoja. Kwa maana kuelekea maisha yenu na Yesu Kristo ni mimi niliyewazaa kwa njia ya kuwatangazia Habari Njema.
Ni kwa sababu hii ninawatumia ninyi Timoteo. Yeye ni mwana wangu mupendwa na mwaminifu mbele ya Bwana. Atawakumbusha kanuni ninazofuata katika maisha yangu na Yesu Kristo, nami ninazofundisha fasi zote katika makanisa yote.
Lakini mimi sikudai hata neno moja ya haki hizo, wala sikuandikii haya kwa kusudi la kutafuta kuzipewa. Ingekuwa heri kwangu kufa kuliko kuzuizwa na mutu yeyote kwamba nisijisifu juu ya jambo hili.
Ninyi munazani kwamba kwa wakati huu wote sisi tunajitetea mbele yenu? Tunasema mambo yale mbele ya Mungu kufuatana na vile tunavyoungana na Kristo. Wandugu wapendwa, mambo yale yote ni kwa kuwajenga ninyi katika imani.
Ni kwa hiyo tunamutangaza Kristo kwa watu wote. Tunaonya na kufundisha kila mutu kwa hekima yote, kusudi tuwasaidie watu wote wapate kufikia kuwa wakamilifu katika kuungana kwao na Kristo.
Watoto wangu wapendwa, ninawaandikia maneno hayo kusudi musitende zambi. Lakini kama mutu akitenda zambi, tuko na yule anayetutetea mbele ya Baba. Naye muteteaji yule ndiye Yesu Kristo, mwenye haki.