Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Tunasumbuka sana tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Wakati tunapotukanwa, tunabariki; wakati tunapoteswa, tunavumilia;

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 4:12
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Heri ninyi, wakati watu wanapowatukana na kuwatesa na kuwasingizia kila namna ya ubaya kwa sababu yangu.


Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.


Halafu Yesu akasema: “Baba uwasamehe, kwa maana hawajui jambo wanalofanya.” Waaskari wakagawanya nguo zake kwa kuzipigia kura.


Muwaombee baraka wale wanaowalaani. Muwaombee wale wanaowaonea.


Mukumbuke maneno niliyowaambia kwamba mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake. Kama walinitesa mimi, watawatesa ninyi vilevile. Na kama walishika maneno yangu, watashika maneno yenu vilevile.


Naye akakaa na kutumika pamoja nao, kwa maana wote walikuwa wafundi wa kutengeneza hema.


Ninyi wenyewe munajua namna nilivyotumika kwa mikono yangu mimi peke kwa kupata vitu vyote ambavyo mimi pamoja na wenzangu tulihitaji.


Kisha akapiga magoti, akalalamika, akisema: “Bwana, usiwahesabie zambi hii.” Na nyuma ya kusema maneno haya, akakufa.


Mumwombe Mungu awabariki wale wanaowatesa; muwaombee baraka wala musiwalaani.


Lakini kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Adui yako akisikia njaa, umupe chakula; kama akisikia kiu, umupe kinywaji. Maana kwa kufanya hivi utamupatisha haya kama vile ungemubebesha makaa ya moto juu ya kichwa.”


Ni nani anayeweza kututenga na upendo wa Kristo? Ni taabu, au huzuni, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kifo?


Au ni mimi na Barnaba tu ndio tunaopaswa kujitumikia wenyewe kwa kupata vifaa vya maisha?


Nilipokuwa nikitumika kati yenu nililipwa na makanisa mengine. Ni kama vile nilinyanganya mali ya makanisa yale na kuitumia kwa kuwasaidia.


Yule aliyekuwa akiiba, asiibe tena, lakini ajikaze kufanya kazi peke yake kwa usawa kusudi apate kuwasaidia wakosefu.


Wandugu, munakumbuka namna tulivyosumbuka na kazi ngumu. Wakati tulipowahubiria Habari Njema ya Mungu, tulitumika muchana na usiku kusudi tusimulemee hata mutu mumoja kati yenu.


Sisi hatukukula chakula cha mutu kwa bure, lakini tulitumika na kuchoka sana. Tulitumika muchana na usiku kusudi tusilemee hata mutu mumoja kati yenu.


Na ni kwa hiyo tunasumbuka na kupigana, kwa maana tunamutumainia Mungu Mwenye Uzima, Mwokozi wa watu wote na hasa zaidi Mwokozi wa waamini.


Wakati walipomutukana, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha watu hata wamwogope. Lakini alijiachilia katika mikono ya Mungu anayehukumu watu kwa haki.


Hata mukiteswa kwa ajili ya haki, ninyi ni wenye heri. Musiwaogope watu, wala musihangaike.


Musirudishiane mabaya kwa mabaya au matusi kwa matusi, lakini muombeane baraka, kwa sababu Mungu aliahidi kuwabariki ninyi wakati alipowaita kumufuata.


Basi watu wanaoteswa kwa ajili ya kufanya mapenzi ya Mungu, waendelee kutenda mema, nao watoe roho yao katika mikono ya Mungu Muumba wao anayekuwa mwaminifu kabisa.


Hata Mikaeli, malaika mukubwa, aliposhindana na kubishana na Shetani juu ya maiti ya Musa, hakusubutu kumuhukumu kwa matusi, lakini alisema: “Bwana mwenyewe akukaripie.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ