Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Yule anayepanda na yule anayenyweshea maji wote ni sawa; naye Mungu atamupa kila mutu mushahara wake kufuatana na kazi aliyofanya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 3:8
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu amesema mara na mara, nami nimesikia tena na tena kwamba uwezo ni wa Mungu.


Anayetunza muti wa tini atakula matunda yake. Anayetumikia bwana wake ataheshimiwa.


Wale wenye hekima watangaa kama vile anga linavyongaa, na wale waliowaongoza wengine kutenda mema, watangaa kama nyota milele.


Kwa maana Mwana wa Mutu atakuja na wamalaika akitukuzwa na Baba yake, halafu atamulipa kila mutu kufuatana na matendo yake.


Naye akamwambia: ‘Nawe vilevile ninakupa utawala juu ya miji mitano.’


Kwa maana Mungu atamulipa kila mutu kwa kadiri ya matendo yake.


Basi wandugu zangu wapenzi, musimame imara bila kutikisika. Muendelee kumutumikia Bwana siku zote, mukijua kwamba masumbuko munayopata kwa ajili ya Bwana hayatapita bure.


Na ikiwa kile mutu alichojenga juu ya musingi huu hakiungui na moto, mutu yule atapokea zawadi.


Hivi yule anayepanda na yule anayenyweshea maji, wote si kitu; Mungu ndiye anayekuwa wa lazima kwa maana ni yeye anayeotesha mbegu.


Kwa maana sisi tunashirikiana na Mungu katika kazi, na ninyi ni shamba la Mungu. Vilevile ninyi ni majengo ya Mungu.


Hivi kuelekea maisha yenu na Kristo, hata mukiwa na walezi maelfu muko tu na baba mumoja. Kwa maana kuelekea maisha yenu na Yesu Kristo ni mimi niliyewazaa kwa njia ya kuwatangazia Habari Njema.


Ni askari gani anayejilipia mwenyewe vifaa vya kiaskari? Au ni muchungaji gani asiyekunywa maziwa ya kundi analochunga?


Kila mutu achunguze mwenendo wake mwenyewe. Basi akiwa na sababu ya kujivuna, ajivune kufuatana na mwenendo wake mwenyewe pasipo kujilinganisha na mutu mwingine.


Kwa maana kila mutu anapaswa kubeba muzigo wake mwenyewe.


Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.


Na wakati Muchungaji Mukubwa atakapotokea, mutapokea taji ya utukufu isiyoweza kuharibika.


Basi, mujiangalie wenyewe, kusudi musipoteze matunda ya kazi yenu, lakini mupokee zawadi kamili.


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Yesu anasema: “Sikiliza, ninakuja upesi! Nitaleta mushahara kwa kulipa kila mumoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ