Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 3:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Mimi nilipanda mbegu na Apolo alinyweshea maji, lakini Mungu ndiye aliyeiotesha.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 3:6
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wimbo wa safari za kidini: wa Solomono. Yawe asipoijenga nyumba, wanaoijenga wanajisumbua bure. Yawe asipoulinda muji, wanaoulinda wanakesha bure.


Musitegemee kutesa, musijisifie mali ya wizi; kama mali zikiongezeka, musizitegemee.


Enyi watu, mutumainie Mungu siku zote; mumufungulie yanayokuwa ndani ya moyo wenu. Yeye ndiye kimbilio letu.


Mutu anayetoa kwa moyo safi atafanikishwa. Mutu anayekunywesha mwingine maji, naye atakunyweshwa.


Hivyo, kama vile udongo unavyootesha mimea, na shamba linavyochipukiza mbegu zilizopandwa humo, Yawe atasababisha haki na sifa kuonekana mbele ya mataifa yote.


Wandugu waamini waliposikia maneno hayo, wakatulia na kumusifu Mungu, wakisema: “Kumbe Mungu amewajalia hata watu wa mataifa mengine vilevile kusudi waweze kugeuka toka zambi na kupata uzima kamili.”


Walipofika Antiokia, wakafanya mukutano wa kanisa na kuwaelezea mambo yote Mungu aliyofanya kwa njia yao, na namna alivyowafungulia watu wa mataifa mengine mulango kusudi wao vilevile wapate kuamini.


Na kati ya wanawake wale kulikuwa mwanamuke mumoja aliyeitwa Ludia, wa muji Tuatera. Yeye alikuwa muchuuzi wa nguo nyekundu za bei kali na mwenye kuogopa Mungu. Mwanamuke yule akatusikiliza kwa maana Bwana alimufungua moyo kusudi apate kufuata kabisa maneno Paulo aliyosema.


Katika siku zile, Muyuda mumoja, jina lake Apolo, muzaliwa wa muji Alesanduria, alikuwa amefika katika muji Efeso. Alikuwa mutu mwenye uwezo katika masemi na mwenye kuelewa sana Maandiko.


Wakati Apolo alipokuwa Korinto, Paulo akasafiri akipitia katika inchi ya vilima na kufika Efeso. Kule akakuta wanafunzi wamoja;


Kisha kuwasalimu, Paulo akaanza kuwaelezea neno kwa neno mambo yote, Mungu aliyofanya kati ya mataifa mengine kwa njia ya kazi yake.


Kwa maana sitasubutu kuongeza kitu kingine, isipokuwa tu kile Kristo alichotimiza kwa njia yangu kusudi watu wa mataifa wapate kumutii Mungu. Alifanya vile kwa njia ya yale aliyoniwezesha kusema na kutenda,


Ninataka kusema: kila mumoja kati yenu anasema maneno yake mbalimbali. Mumoja anasema: “Mimi ni wa Paulo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Petro,” na mwingine anasema: “Mimi ni wa Kristo.”


Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.


ikiwa Paulo, Apolo au Petro, dunia, uzima, kifo, mambo ya sasa au mambo yatakayokuja.


Hivi yule anayepanda na yule anayenyweshea maji, wote si kitu; Mungu ndiye anayekuwa wa lazima kwa maana ni yeye anayeotesha mbegu.


Mimi si huru? Mimi si mutume? Mimi sikumwona Yesu Kristo Bwana wetu? Ninyi si matunda ya kazi yangu kwa ajili ya Bwana?


Hivi Kristo apate kukaa ndani ya mioyo yenu kwa njia ya imani, nanyi mupate kuwa na mizizi na musingi katika upendo.


Kwa maana tulipohubiri Habari Njema kwenu, hatukuihubiri kwa maneno tu, lakini kwa uwezo na kwa musaada wa Roho Mutakatifu na kwa uhakika kabisa. Munajua namna gani tulivyoishi katikati yenu, kusudi tupate kuwafalia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ