Ninataka kusema: kila mumoja kati yenu anasema maneno yake mbalimbali. Mumoja anasema: “Mimi ni wa Paulo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Petro,” na mwingine anasema: “Mimi ni wa Kristo.”
kwa sababu mungali munatawaliwa na mambo ya kidunia. Kwa maana ikiwa kungali wivu na ugomvi katikati yenu, haionyeshi kwamba munatawaliwa na mambo ya kidunia, nanyi munaishi kufuatana na hali ya kimutu?
Wandugu zangu, nimesema maneno haya nikitwaa mufano wa Apolo na wangu mimi mwenyewe kusudi yakuwe fundisho kwenu. Nilitaka kwamba kufuatana na mufano huu mujifunze maana ya masemi haya: “Musipite pembeni ya maandiko.” Hata mutu mumoja kati yenu asijivunie mutu fulani na kuzarau mwingine.