Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma.
Maana kama tunaishi, tunaishi kwa ajili ya Bwana, na kama tunakufa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi ikiwa tunaishi, au ikiwa tunakufa, sisi ni watu wa Bwana.
Na wakati vitu vyote vitakapokuwa vimewekwa chini ya mamlaka ya Mwana, halafu yeye mwenyewe atajiweka chini ya mamlaka ya Mungu aliyemupa mamlaka juu ya vitu vyote, kusudi Mungu apate kutawala juu ya vyote kabisa.
Ingawa hivi, kwa ngambo yetu sisi tuko na Mungu mumoja peke yake tu, ndiye Baba aliyeumba vitu vyote, nasi tunaishi kwa nguvu yake. Vilevile kuko Bwana mumoja tu, ndiye Yesu Kristo. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, nasi tunaishi kwa nguvu yake.
Ninyi munaangalia tu namna vitu vinavyoonekana kwa inje. Mutu yeyote anayejiaminia kwamba yeye ni wa Kristo, inafaa afikiri tena yeye mwenyewe mambo haya: ikiwa yeye ni wa Kristo sisi vilevile ni wa Kristo.