Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 3:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Mutu anaweza kujenga juu ya musingi huu na zahabu, feza, mawe ya bei kali, miti, nyasi au majani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 3:12
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sheria uliyoweka ni bora kwangu, kuliko mali zote za dunia.


Kumutii Yawe ni jambo jema; kunadumu milele. Maagizo ya Yawe ni sawa, yote ni ya haki kabisa.


Basi, watu wote wakatawanyika kila pahali katika inchi ya Misri wakitafuta nyasi za kutengeneza matofali.


Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.


Usiongeze neno katika maneno yake, kusudi asikukaripie, nawe usionekane kuwa mwongo.


Chagua mafundisho yangu pahali pa feza; na maarifa pahali pa zahabu safi.


Pahali pa shaba nitakuletea zahabu, pahali pa chuma nitakuletea feza, pahali pa miti, nitakuletea shaba, na pahali pa mawe nitakuletea chuma. Amani itatawala juu yako, haki itakuongoza.


Nabii aliyeota ndoto, atangaze ndoto yake, lakini yule aliyefunuliwa ujumbe wangu autangaze kwa uaminifu. Kuna ulinganifu gani kati ya maganda na ngano? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Na hata kati yenu kutatokea watu watakaotoa mafundisho ya kupotosha wengine kusudi wawavute waamini kuwafuata.


Wandugu zangu, ninawasihi, mufanye angalisho na wale wanaoleta matengano na mambo ya kuwapotoa wengine wakipinga mafundisho muliyopokea. Mujitenge mbali nao.


Kwa maana hakuna mutu anayeweza kuweka musingi mwingine pahali pa ule uliokwisha kuwekwa, ni kusema Yesu Kristo.


Lakini hali ya kazi ya kila mutu itaonekana wazi, kwa sababu Siku ile ya hukumu itaionyesha waziwazi. Kwa maana Siku ile itajitokeza katikati ya moto, na moto ule ndio utakaopima na kuonyesha hali ya kazi ya kila mutu.


Basi sisi si kama wengine wengi wanaochuuza neno la Mungu; lakini kwa sababu Mungu ndiye aliyetutuma, sisi tunasema ukweli mbele yake, kama vile watumishi wa Kristo.


Tumekataa mambo ya kisirisiri na ya haya. Hatuna mwenendo wa udanganyifu wala hatupotowi neno la Mungu. Lakini tunajulisha waziwazi ukweli kusudi tuvute kila mutu kutuaminia katika zamiri yake mbele ya Mungu.


Mujiangalie hata mutu asiwapotoshe kwa elimu yake ya udanganyifu mutupu inayotegemea desturi za watu na roho mbaya zinazotawala dunia, lakini haitegemei mafundisho ya Kristo.


Kama mutu akifundisha mafundisho mengine, naye hakubali maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo wala mafundisho yanayolingana na dini yetu,


Ndani ya nyumba kubwa, hamuna vyombo vya zahabu na feza tu, lakini muko vilevile vyombo vya miti na vya udongo. Vimoja ni vya matumizi ya kipekee na vingine ni vya matumizi ya kawaida.


Lakini watu waovu na wadanganyifu wataendelea katika maovu, wakipotosha watu wengine na kujipotosha wenyewe.


Wanawake wale wanataka kujifunza siku zote, lakini hawafikii kutambua ukweli.


Maana kutakuja wakati watu watakapokataa kusikiliza mafundisho ya kweli, lakini watafuata tamaa zao wenyewe wakijitafutia walimu wengi kwa kuwafundisha mambo yale wanayotamani kusikia.


Musidanganywe na mafundisho mengine ya kigeni ya kila namna. Kwa maana mioyo yetu inapaswa kutiwa nguvu kwa njia ya neema ya Mungu, wala si kwa njia ya kushika kanuni zinazoagizwa juu ya vyakula. Kanuni hizo haziwafalii kitu wale wanaozishika.


Majaribu hayo ni kwa ajili ya kupima imani yenu. Zahabu ni kitu kinachoharibika, lakini ingawa vile inapimwa kwa njia ya kuchomwa ndani ya moto. Hivi vilevile imani yenu inayokuwa ya bei kali kuliko zahabu, inapaswa kupimwa kusudi ijulikane kuwa ya kweli. Na kwa sababu hii mutapata sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atakapotokea.


Lakini niko na neno hili juu yako: kati yako kuna watu wamoja wanaoshika mafundisho ya Balama. Huyu ndiye aliyemufundisha Balaka kwamba awapime Waisraeli, kusudi wakule vyakula vya kutambikia sanamu za miungu na kufanya uasherati.


Ukuta ulikuwa umejengwa na mawe ya bei kali ya yaspi, na muji wenyewe ulikuwa umejengwa na zahabu safi inayongaa kama kioo.


Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ