Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Wakorinto 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kwa kadiri ya zawadi Mungu aliyonipatia, kama vile fundi wa kujenga mwenye hekima, niliweka musingi. Na sasa, mutu mwingine anajenga juu yake. Lakini inafaa kila mutu aangalie vizuri namna anavyojenga.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Wakorinto 3:10
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa ninakutumia fundi mwenye ujuzi sana na mwenye akili, jina lake Huruma-Abi.


Watu wote wenye ujuzi waliokuwa wanafanya kazi za kila namna za kujenga hema la mukutano walitoka, kila mumoja katika kazi yake, wakamwendea


Mutu anasifiwa kadiri ya hekima yake, lakini mwenye moyo wa mafikiri mabaya anazaruliwa.


Hekima amejenga nyumba yake, nyumba yenye nguzo saba.


Basi, zaidi ya kuwa na hekima yake, Muhubiri aliendelea kuwafundisha watu ujuzi. Alipima, akachunguza na kutia kwa usawa mezali kwa ufundi mwingi.


Wale wenye hekima watangaa kama vile anga linavyongaa, na wale waliowaongoza wengine kutenda mema, watangaa kama nyota milele.


Zerubabeli ameuweka musingi wa hekalu naye vilevile atalikamilisha. Hayo yatakapotukia, watu wangu watajua kwamba mimi Yawe wa majeshi ndimi niliyekutuma kwao.


“Basi ni nani anayekuwa mutumishi mwaminifu na mwenye akili? Ni yule bwana wake aliyemuweka kuwa musimamizi wa watumishi wake wengine na kumwamuru kuwapatia posho yao kwa wakati uliopangwa.


“Basi kila mutu anayesikia hayo maneno yangu na kuyashika, anafananishwa na mutu mwenye akili aliyejenga nyumba yake juu ya jiwe.


Ujiangalie vizuri kusudi mwangaza unaokuwa ndani yako usigeuke kuwa giza.


Yesu akawajibu: “Muangalie vizuri, musidanganywe. Watu wengi watakuja wakijiita kwa jina langu, wakisema kwamba wao ndio Kristo, nao wakati umetimia. Ingawa vile, musiwafuate.


Apolo alipotaka kwenda katika jimbo la Akaya, wandugu waamini wakamutia moyo, nao wakawaandikia wanafunzi wa kule kwamba wamukaribishe vizuri. Na wakati alipofika kule, akawasaidia sana wale walioamini kwa nguvu ya neema ya Mungu,


Kwa njia yake Mungu amenipa neema ya kuwa mutume kusudi niongoze mataifa yote yapate kumwamini na kumutii. Na kwa tendo hilo jina lake lipate kusifiwa.


Kufuatana na neema niliyopewa na Mungu, ninawaambia ninyi wote: mutu asijiwazie kuwa na ukubwa kupita vile inavyomustahili. Lakini mukuwe na mawazo ya ukadirifu, kila mumoja kulingana na kipimo cha imani aliyopewa na Mungu.


Lakini mara moja moja nimewaandikia kwa uhodari juu ya mambo fulani kusudi niwakumbushe tena mambo yale. Nimefanya vile kutokana na neema ile niliyopewa na Mungu


Nayo nia moja niliyokuwa nayo ni kuhubiri tu Habari Njema fasi zote ambapo habari za Kristo zilipokuwa hazijasikilika bado. Nilikusudia vile kusudi nisijenge juu ya musingi uliowekwa na mutu mwingine,


Kwa maana hakuna mutu anayeweza kuweka musingi mwingine pahali pa ule uliokwisha kuwekwa, ni kusema Yesu Kristo.


Hata ikiwa watu wengine hawakubali kuwa mimi ni mutume, ninyi munakubali kuwa mimi ni mutume. Ninyi ni kitambulisho kinachohakikisha kwamba mimi ni mutume, kwa ajili ya kuungana kwenu na Bwana.


Basi, hatujivuni kupita kipimo juu ya kazi ya watu wengine. Lakini tunatumaini kwamba imani yenu itakapokuwa ikiongezeka, tutaweza kufanya kazi kubwa zaidi kati yenu kufuatana na kipimo cha kazi tuliyopewa na Mungu.


Ninyi vilevile ni kama jengo linalosimama juu ya musingi uliowekwa na mitume na manabii; Yesu Kristo mwenyewe ndiye jiwe kubwa la pembe.


Ni kwa sababu hiyo ninatumika na kupigana kwa uwezo ninaopewa na Kristo, unaoniwezesha kufanya kazi kwa nguvu.


Mumwambie Arkipo aangalie vizuri atimize kazi ile aliyopewa na Bwana.


na kumutuma ndugu yetu Timoteo, anayemutumikia Mungu pamoja nasi katika kazi ya kutangaza Habari Njema ya Kristo. Tulimutuma kwenu apate kuwatia nguvu na kuwafariji katika imani yenu,


Ujiangalie wewe mwenyewe na kuangalia mafundisho yako, nawe ushikamane nayo. Kwa maana ukifanya hivi, utajiokoa wewe mwenyewe na kuokoa wale wanaokusikiliza.


Ufanye juhudi kusudi upate kuhesabiwa mbele ya Mungu kama mutu anayemupendeza, ukiwa kama mutumishi asiyesikia haya juu ya kazi yake, lakini anayetangaza kwa haki ujumbe wa kweli wa Mungu.


Wandugu zangu, kati yenu kusikuwe walimu wengi, kwa maana munajua vema ya kuwa sisi walimu tutahukumiwa vikali zaidi kuliko watu wengine.


Yule anayehubiri, anapaswa kutoa ujumbe wa Mungu. Na yule anayetumika, atumike kwa kadiri ya nguvu alizopewa na Mungu, kusudi Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa njia ya Yesu Kristo anayekuwa mwenye utukufu na uwezo kwa milele na milele. Amina.


Mutambue kwamba njia ya kuvumilia kwa Bwana wetu ni wakati muzuri anaowapatia kusudi mupate kuokolewa. Na hiyo ni kufuatana na vile ndugu yetu mupendwa Paulo alivyowaandikia akiongozwa na hekima aliyopewa na Mungu.


Na ukuta uliozunguka muji ule ulikuwa umejengwa juu ya mawe ya musingi kumi na mawili na juu ya kila jiwe kulikuwa kumeandikwa jina la kila mumoja wa mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.


Musingi wa ukuta uliozunguka muji ule ulikuwa unapambwa na mawe ya bei kali ya kila aina. Mawe ya musingi wa kwanza ulikuwa wa mawe ya yaspi, wa pili wa mawe ya safilo, wa tatu wa mawe ya kaledoni, wa ine wa mawe ya zumaridi,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ