Ninasikia watu wengi wakinisingizia uongo, nao wananipanga jina la Kitisho Kila Pahali! Wengine wanasema: Tumushitaki, Tumushitaki! Rafiki zangu wapenzi wote wanangojea kwa hamu nianguke! Wanasema: Labda atadanganyika, tupate kumunasa na kumulipiza kisasi.
Maono yao ni ya uongo mutupu na wanachotabiri ni udanganyifu mutupu. Wanasema “Ni ujumbe wa Yawe” lakini Yawe hakuwatuma; kisha wanamutazamia atimize yale wanayosema.
Basi, Mungu anayekuwa musingi wa matumaini, awajaze furaha kamili na amani kutokana na imani yenu; hata tumaini lenu lipate kuongezeka kwa nguvu ya Roho Mutakatifu.
kwa njia ya uwezo wa vitambulisho na maajabu, na kwa uwezo wa Roho Mutakatifu. Hivi tokea Yerusalema mpaka kufika katika jimbo la Iliriko nimehubiri fasi zote Habari Njema ya Kristo.
Kwa maana watu wa namna hii hawamutumikii Bwana wetu Kristo, lakini wanatumikia tu tumbo yao wenyewe. Tena kwa maneno yao matamu na ya kujipendekeza wanadanganya watu wasiokuwa na makosa.
Kristo hakunituma kwa kubatiza, lakini amenituma kwa kutangaza Habari Njema. Amenituma kuitangaza bila kutumia hekima ya usemi, kusudi uwezo unaotokana na kufa kwa Kristo juu ya musalaba usihesabiwe kuwa bure.
Nasi tunaposema hatutumii maneno yanayotokana na hekima ya kimutu, lakini maneno yanayotokana na Roho wa Mungu, tukieleza maneno ya kiroho kwa watu wanaokuwa wa Roho.
Tunaonyesha kwamba sisi ni watumishi wa Mungu kwa njia ya usafi wa moyo wetu, ya ufahamu, ya uvumilivu, ya wema wetu, ya Roho Mutakatifu, ya upendo wetu wa kweli,
Basi kusema vile inaonyesha kwamba ninatafuta watu wanikubali? Hapana! Ninataka kukubaliwa na Mungu. Au ninatafuta kuwapendeza watu? Kama ningekuwa ningali ninatafuta kuwapendeza watu, singekuwa mutumishi wa Kristo.
Kwa maana tulipohubiri Habari Njema kwenu, hatukuihubiri kwa maneno tu, lakini kwa uwezo na kwa musaada wa Roho Mutakatifu na kwa uhakika kabisa. Munajua namna gani tulivyoishi katikati yenu, kusudi tupate kuwafalia.
Mungu aliwafunulia wale manabii kwamba ujumbe ule walioutangaza haukuwaelekea wao wenyewe, lakini uliwaelekea ninyi. Na sasa ujumbe ule umetangazwa kwenu na wale waliowahubiri Habari Njema kwa uwezo wa Roho Mutakatifu aliyetumwa toka mbinguni. Hata wamalaika vilevile wanatamani kujua mambo hayo.
Basi, wakati tulipowajulisha uwezo na kurudia kwa Bwana wetu Yesu Kristo, sisi hatukutumia hadisi za uongo zilizotungwa kwa werevu. Lakini tulijionea na macho yetu sisi wenyewe uwezo wake.
Kwa maana kwa masemi yao ya kujivuna na yasiyokuwa na maana, na kwa njia ya tamaa zao mbaya za kimwili, wanawavuta watu ambao wanaanza kuwaepuka, na wale wanaoishi katika udanganyifu.
Basi siku ya ine wakamwambia muke wa Samusoni: “Umubembeleze mume wako kusudi atuambie maana ya kitendawili hicho, kama sivyo tutakuteketeza kwa moto wewe pamoja na nyumba ya baba yako. Ninyi mulitualika hapa kutunyanganya mali zetu?”
Wakubwa wa Wafilistini wakamwendea Delila, wakamwambia: “Umubembeleze Samusoni kusudi ujue asili ya nguvu zake nyingi kusudi tuweze kumukamata na kumufunga. Ukifanya hivyo, kila mumoja wetu atakupa vikoroti makumi tatu vya feza.”